Jumamosi, 31 Desemba 2011

HERI YA MWAKA MPYA 2012.

IT IS HEREBY SUBMITTED THAT  2011 HAS BEEN OVERTAKEN BY EVENTS, THEREFORE IT IS WITHDRAWN AND 2012 IS FILED.WITHOUT PREJUDICE TO THE FOREGOING, I DISPUTE ALL CLAIMS THAT 2011 IS THE END OF EVERYTHING. JUST FORGET AND FORGIVE THE PAST, LIFE GOES ON. MAY 2012 COMES WITH REVOLUTION, BE BLESSED. I ALSO SUBMIT THAT THE READER OF THIS MESSAGE WHETHER IS A LEARNED FRIEND OR A LAYMAN, THE AFFIDAVIT OF OUR FRIENDSHIP, PRAYERS AND GOOD WISHES FOR THE NEW YEAR 2012 IS ATTACHED HEREWITH, I CRAVE LEAVE FOR IT TO BE CONSTRUED AS PART OF THESE GREETINGS.

BALOZI SEFUE AMEAPISHWA LEO IKULU KUSHIKA WADHIFA MPYA WA UKATIBU MKUU.

Hapa Balozi akisubiri shughuli za kuapishwa zianze rasmi.

Rais Jakaya M. Kikwete akimwapisha Balozi Ombeni Sefue kuwa Katibu Mkuu leo asubuhi Ikulu Dar es Salaam.

BALOZI OMBENI SEFUE ATEULIWA KUWA KATIBU MKUU KIONGOZI, KUMRITHI LUHANJO.

Balozi Ombeni Sefue, Katibu Mkuu Kiongozi mpya, kabla ya kuteuliwa alikuwa Balozi wa Tanzania nchini Marekani.

NAIBU WAZIRI WA ELIMU AGAWA LAPTOP KWA WANAFUNZI WA CHUO KIKUU HURIA CHA TANZANIA(OUT)

DIRECTORATE OF COMMUNICATIONS AND MARKETING
ANNOUNCEMENT
LAUNCH OF LAPTOP PROJECT FOR STUDENTS AND
STAFF IN HIGHER LEARNING INSTITUTIONS
This is to inform students and staff in Higher Learning Institutions,
who deposited their funds for the purpose of purchasing laptops for
assisting their learning/teaching through the Open University
Students Organization (OUTSO) that the laptops will be distributed on
Friday December 30
The distribution of the laptops will be launched by the Deputy Minister
for Education and Vocational Training, Hon. Phillipo Mulugo, MP.



Naibu Waziri wa Elimu akizindua mradi wa kuwagawia wanafunzi wa Chuo Kikuu Huria cha Tanzania Laptops jana katika Hotel ya Serena Dar es Salaam,kushoto ni Makamu Mkuu wa Chuo hicho Profesa Tolly Mbwete. Kompyuta hizi zimeuzwa kwa bei raisi ya shilingi laki nne na nusu tu toka kampuni ya Royal Mark ya Dar es salaam.

THE OPEN UNIVERSITY OF TANZANIA

Ijumaa, 30 Desemba 2011

MTANGAZAJI MAARUFU WA ITV NA BAADAE BBC AFARIKI DUNIA LEO HII, NI JOHN NGAHYOMA.

Mpiganaji John Ngahyoma afariki dunia
HABARI ILIYOTUFIKIA HIVI PUNDE INAELEZA KUWA,ALIYEKUWA MTANGAZAJI WA ITV/RADIO ONE MIAKA YA NYUMA NA BAADAE KUHAMIA KWENYE SHIRIKA LA UTANGAZAJI LA UINGEREZA (BBC),BW. JOHN NGAYOMA AMEFARIKI DUNIA MAPEMA LEO ASUBUHI.
HAYATI NGAHYOMA AMBAYE AMEFIKWA NA MAUTI LEO AKIWA HOSPITALI AMBAKO ALIKUWA AKIPATIWA MATIBABU YA MARADHI YALIYOKUWA YAKIMSUMBUA KWA MUDA MREFU AMBAPO ALIENDA MPAKA NCHINI INDIA KWA MATIBABU YA MARADHI YAKE HAYO BILA MAFANIKIO.
MSIBA UPO NYUMBANI KWA MAREHEMU MAENEO YA TABATA SEGEREA NA TARATIBU ZOTE BADO ZINAENDELEA KUFANYIKA.

MBUNGE ASEMA RAIS MUGABE NI SHOGA.

Rais Robert Mugabe wa Zimbabwe.
Mbunge wa chama cha MDC (Movement for Democratic Change) cha nchini Zimbabwe amejikuta akiingia matatani baada ya kudai rais wa Zimbabwe, Robert Mugabe alifanya mapenzi ya jinsia moja.Mbunge huyo ametupwa jela kwa siku saba.

Mbunge huyo wa kike aliyetajwa kwa jina la Lynette Kareny alisema kuwa Robert Mugabe ambaye pia ni rais wa chama tawala cha Zanu-PF alifanya mapenzi na wanasiasa wawili wa kiume.

"Karenyi anatuhumiwa kutoa kauli hiyo ya kumkashifu kiongozi wa nchi wakati wa mkutano wa hadhara wa chama cha MDC uliofanyika disemba 9 kwenye viwanja vya mpira vya Chimanimani,” limeripoti gazeti la The Herald la nchini Zimbabwe

Alhamisi, 29 Desemba 2011

MALKIA WA MIPASHO AL ANISA HADIJA KOPA KUTUMBUIZA NACHINGWEA LINDI MWAKA MPYA TAREHE 02.



Malkia Hadija Kopa.


Kundi zima la TOT Taarab chini ya uongozi wa Al Anisa Khadija Bint Kopa linatarajiwa kutumbuiza mjini Nachingwea siku ya pili baada ya mwaka mpya kuingia yaani tarehe 02/01/2012 ikiwa ni shamrashamra za kuukaribisha mwaka 2012 katika Ukumbi maarufu wa Nachingwea Resort (NR).Wakati wakazi wa Nachingwea wakisubiri kwa hamu kumuona Malkia na kundi lake la TOT, kwa sasa Hadija yupo katika ziara ya nchi kadhaa za Ulaya, lakini kwa mujibu wa waandaaji wa ziara hiyo,wamesema hilo lisiwatishe na wana uhakika kuwa Hadija atakuwepo siku hiyo ili kuwaburudisha.

Jumatano, 28 Desemba 2011

MAHAKAMA YASEMA KAFULILA BADO MBUNGE HALALI

MAHAKAMA Kuu imetoa amri kusitisha kutekelezwa kwa uamuzi wa Halmashauri Kuu ya
Chama cha NCCRMageuzi wa kumfukuza uanachama Mbunge wa Kigoma Kusini, David Kafulila
hadi kesi aliyofungua itakapomalizika.

Uamuzi huo ulitolewa jana katika Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam na Jaji Alise Chingwile kutokana na maombi ya zuio yaliyowasilishwa na Kafulila kupitia Kampuni ya Uwakili ya Asyla ya Dar es Salaam.
David Kafulila
Wakili wa Kafulila kutoka kampuni hiyo, Daniel Welwel alisema maombi hayo waliyawasilisha Ijumaa iliyopita chini ya hati ya dharura, kupinga kuvuliwa uanachama.

Kwa mujibu wa Wakili huyo, katika maombi hayo, walidai kwamba uamuzi huo wa NCCR-Mageuzi ukitekelezwa dhidi ya Kafulila atakuwa amekosa sifa za ubunge na jimbo litakosa mbunge.

“Tukasema na kesi ya msingi itakuwa haina maana,” alidai Wakili wa mwanasiasa huyo kijana
aliyewahi pia kuwa mwanachama na kiongozi wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema).

Katika kesi ya msingi ambayo itatajwa Februari 21, mwakani, Kafulila kupitia kwa mawakili wake, anadai uamuzi wa NCCR Mageuzi haukuwa halali kwa sababu Katiba ya chama hicho haikufuatwa.

Vile vile anadai hakupewa haki ya kusikilizwa licha ya kwamba ni haki yake ya msingi.

Anadai pia kwamba wajumbe walioshiriki kupitisha uamuzi huo, wengine hawakuwa wajumbe halali.

Watu wanaomuunga mkono pamoja na walio karibu na mbunge huyo, akiwemo Mbunge wa Kigoma Kaskazini, Kabwe Zitto (Chadema), wameelezea kufurahishwa na uamuzi huo wa Mahakama.

“Kafulila kuendelea na ubunge..... Mahakama Kuu imetoa amri muda mfupi uliopita.

Ataendelea kuwa Mbunge mpaka hapo kesi ya msingi itakapokwisha. Mungu yupo pamoja na wanyonge siku zote,” alisema Zitto kupitia mtandao wa kijamii.
.”

Awali, Katibu wa Bunge, Dk. Thomas Kashilillah alikiri kwamba ofisi imekwishapokea barua ya
NCCR Mageuzi ya kumvua ubunge Kafulila na kwamba inafanyiwa kazi, ingawa hakuna muda maalumu wa kutenda kazi hiyo

PAMOJA NA UTUKUTU WAKE MARIO BALOTELLI ACHANGIA KANISANI KWAKE SHILINGI LAKI TANO WAKATI WA MKESHA WA KRISMASI.

Some footballers enjoy the glitz and glamour of Christmas and are seen attending celebrity parties or enjoying a lavish day at home with the family. But one Manchester City player decided to give something back to his fans this Yuletide - including a charitable church donation and a huge round of drinks.
According to reports today, Mario Balotelli was seen at St John's Church in Chorlton, Manchester, on Christmas Eve to attend the midnight Mass service.
Generous: Manchester City striker Mario Balotelli was full of Christmas cheer as he donated to his local church and bought an expensive round of drinks for patrons at his local pub
Generous: Manchester City striker Mario Balotelli was full of Christmas cheer as he donated to his local church and bought an expensive round of drinks for patrons at his local pub
Accompanied by his girlfriend, they stayed for the carols and after the service, Balotelli put £200 in the collection tray.
A source told The Sun: 'Nobody could believe it when he walked in.
'The last thing anyone expected was a big celebrity like him turning up for the service but he was very polite and charming and didn't draw attention to himself.'
Donation: This is St John's church in Chorlton where Mario put £200 in the collection box after the midnight Mass service
Donation: This is St John's church in Chorlton where Mario put £200 in the collection box after the midnight Mass service

The 21-year-old had been feeling in a generous and festive mood all day as earlier he had visited the Tudor pub in the Manchester suburb of Peel Hall.
He chatted to patrons, had his picture taken with some of them - and then put £1,000 behind the bar.
A source told the paper: 'He was very down to earth. Everyone wanted to talk to him and he took it in his stride.
'It's not a smart pub, so it was a big surprise when he walked in.'
Down to earth: Before the church service, Mario dropped in to the Tudor pub and put £1,000 behind the bar
Down to earth: Before the church service, Mario dropped in to the Tudor pub and put £1,000 behind the bar.

WACHEZAJI YANGA NJAA KALI, PESA HAKUNA.

Wachezaji Yanga walia njaa


Timu ya Yanga
Ikiwa inakabiliwa na ushindani mkali katika kampeni yake ya kutetea ubingwa wa Ligi Kuu ya Tanzania Bara na pia mashindano ya Klabu Bingwa Afrika, programu za mazoezi ya Yanga inashindwa kutekelezeka kikamilifu kutokana na wachezaji wake kutopata mishahara yao ya miezi miwili.
Mishahara hiyo ambayo wachezaji wanadai ni ya mwezi Novemba na Desemba, ambao umeambatana na sikukuu ya Krismasi na mwaka mpya.
Kwa mujibu wa habari ambazo gazeti hili imezipata ni kwamba mbali na wachezaji hao, pia wafanyakazi wengine walioajiriwa na klabu hiyo hawajalipwa kwa muda wa miezi mitatu sasa.
Chanzo hicho kiliongeza kuwa hali hiyo ya ukata imechangia mambo mengi kutofanyika kama ilivyotarajiwa ikiwemo kuvurugika kwa programu ya mazoezi.
"Hali ni mbaya, klabu haina pesa, mambo mengi hayafanyiki kama ilivyokusudiwa, tunajaribu kufanya kila linalowezekana ili kutatua tatizo hili linalotukabili," alisema mmoja wa viongozi wa Yanga ambaye hakutaka jina lake litajwe.
Aliongeza kuwa kukosekana kwa fedha kutoka kwa aliyekuwa mfadhili wao na mapato madogo ya mlangoni yaliyokuwa yakipatikana katika mechi za mzunguko wa kwanza wa ligi ndio sababu nyingine iliyofanya klabu yao ikose fedha za kujiendesha.

Jumanne, 27 Desemba 2011

MSONDO NA SIKINDE WAPAGAWISHA MASHABIKI MKESHA WA XMASS CHINI YA UDHAMINI WA KONYAGI

Mpambano huo ulivuta mashabiki wengi katika viwanja vya TCC Sigara ambapo bendi ya Sikinde, ilionekana kuwapiku wenzao wa Msondo kutokana na Shamrashamra zilizokuwa zikitawala wakati Msondo wakiimba jukwaani, Onyesho hilo limefanyika usiku wa kuamkia jana ikiwa ni pamoja na kusherehekea sikukuu ya Krismas.
Wanamuziki Shaban Dede na TX Moshi William Junior wa Msondo wakiimba jukwaani huku mashabiki wakiwashangilia kwelikweli wakati wa onyesho hilo lililofanyika TCC Chang'ombe usiku wa kuamkia jana.
TX Moshi William Junior akiimba katikati ya mashabiki , huku mashabiiki hao wakimshangilia.
Kutoka kulia ni mwimbaji wa Bendi ya Sikinde Hassan Kunyata, Yusuph Bernald na Shaban Lendi wapiga Saxaphone wakifanya vitu vyao jukwaani.
Mwimbaji wa bendi ya Sikinde Abdallah Hemba akicheza sambamba na wanenguaji wa bendi hiyo wakati bendi hiyo ilipotupa karata yake ya mwisho usiku wa kuamkia leo

RASHID MATUMLA NA MANENO OSWALD HAKUNA MBABE.

MANENO OSWARD VS RASHIDI MATUMLA HAKUNA MBABE KILA MMOJA ATOKA NA POINTI 99

Bondia Rashidi Matumla (kushoto) akiwa chini baada ya kuteleza uku mpinzani wake Maneno Osward akimsubili kwa ajili ya kumpiga wakati wa mpambano wao uliofanyika Dar es salaam jana wakati wa sikukuu ya Xmasi mpaka mwisho wa pambano point ni 99 kwa 99 hivyo kuwa droo.(Picha na www.superdboxingcoach.blogspot.com)
Bondia Rashidi Matumla (kushoto) na Maneno Osward wakioneshana ufundi wa kutupa masumbwi wakati wa mpambano wao uliofanyika Dar es salaam jana wakati wa sikukuu ya Xmasi mpaka mwisho wa pambano pointi ni 99 kwa 99 hivyo kuwa droo

UKATILI WA AJABU, MJOMBA AMUUNGUZA MTOTO KWA MOTO MAKUSUDI.

Mjomba wa mtoto aliyeunguzwa moto.
 
Mtoto aliyeunguzwa moto.
 
 
Na, Gordon Kalulunga, Mbeya

MTOTO Oscar Oliver (17) mkazi wa Ilemi Jijini Mbeya amechomwa kiganja chake cha mkono wa kushoto na kaa la moto kwa kulazimishwa na mjomba wake akituhumiwa kuwa hana tabia njema.

Tukio hilo la kinyama limetokea usiku wa kuamkia siku ya sikukuu ya Kristmas nyumbani kwa Andendekisye Mwakabubu (30) ambaye ndiye anayedaiwa kufanya unyama huo kwa mpwa wake akimtuhumu kuwa alitaka kumwibia.

Mwakabubu anadaiwa kumlazimisha mtoto huyo kushika kaa la moto na baada ya mtoto huyo kuungua kiganja chake alimpeleka katika kituo kidogo cha polisi cha Mwanjelwa na kumfunmgulia kesi ya wizi wa kuibiwa vitu mbalimbali ili kuweza kuficha unyama wake huo.

Baada ya kufungua kesi hiyo, askari polisi walimshikilia kijana huyo na kumpeleka katika kituo kikuu cha polisi mkoani hapa na kumweleza mlalamikaji huyo bandia kuwa alitakiwa kufika kituoni hapo kwa ajili ya mtoto huyo kupelekwa mahakamani.

Mtoto huyo alipofikishwa katika kituo hicho kikuu alikutana na askari waliopo ndani ya kitengo cha kuelimisha jamii kuhusu unyanyasaji wa kijinsi hususani kwa watoto ambao walimsikiliza mtoto huyo na hatimaye jana walimwita mpwa wake kwa ajili ya kutoa maelezo.

Mwakabubu baada ya kufika kituoni hapo na kutoa maelezo na kuulizwa kuwa nani aliyehusika na tukio hilo alishindwa kubainisha huku akisema kuwa hajui aliyemchoma huku akisahau kuwa katika maelezo yake ya awali yeye ndiye alikuwa mlalamikaji jambo ambalo liliwashawishi askari hao kumakamata na kumpeleka rumande.

Mpwa huyo wa mtoto Oscar akiwa mahabausu ya kituo hicho cha polisi, askari hao wanaunda mtandao huo wa kuelimisha jamii juu ya unyanyasaji wa kijinsia mkoani hapa hususani kwa watoto walimchukua mtoto huyo na kumpeleka Hospitalini kwa ajili ya matibabu.

Mwakabubu alihojiwa na askari wa mtandao huo wakiongozwa na askari aliyefahamika kwa jina la Pudensiana Baito huku mwandishi wa habari hizi akiwa anafuatilia tukio hilo na askari huyo alipotakiwa kueleza kwa undani tukio hilo alisema kuwa yeye si msemaji wa jeshi la polisi.

MCHUNGAJI LUSEKELO AGEUKA HAKIMU, ASEMA JAIRO NA LUHANJO HAWANA MAKOSA!!!!!!!

 
Picture
Mchungaji Kiongozi wa Kanisa la Maombezi (GRC) lililopo Ubungo Dar es Saama, Mchungaji Antony Lusekelo, ameibuka na kusema kuwa sakata la Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini Bw. David Jairo, na Katibu Mkuu Kiongozi Bw. Philemon Luhanjo, ni majungu na haina tatizo.

Bw. Jairo anadaiwa kuchangisha fedha za umma kwa ajili ya kugharamikia kupitisha bajeti ya wizara hiyo kinyume cha utaratibu huku Bw. Luhanjo akidaiwa kumjingia kifua.

Mchungaji Lusekelo maarufu kama Mzee wa Upako amesisitiza kuwa wapo viongozi wengi waliofanya kitendo sawa na ya  Jairo lakini hayajulikani hivyo kutaka Watanzania kuacha tabia ya kuchafuana.

Akizungunza na waandishi wa habari Kanisani kwake jana, Mchungaji Lusekelo alisema haiwezekani mtu mmoja kupanga kuchangisha fedha za wizara bila kuwa na mtandao na viongozi wengine na kudai kuwa kilichotokea ni siri kuvuja na si vinginevyo, "Ninachojua ni kwamba wezi wote wako mahakamani, unapoona mtu analalamikiwa kila siku wala hakamatwi ujue ni majungu tu na mambo hayo hafanyi, angefanya angekuwa selo

Ikumbukwe kwamba kuharibiana na kuchafuana kupo, mfano mimi niliwahi kuambiwa kwamba nimeenda nchini Nigeria kutafuta nguvu za giza wakati sijawai hata kuwaza kufanya kitendo cha namna hiyo,"alisema Mchungaji Lusekelo na kuendelea "Lazima tukiri kwamba watu wanachafuana na ndio maana ninasema hata kwa Bw. Jairo ni siri tu ilivuja na hawezi kufanya peke yake," alisisitiza

Jumapili, 25 Desemba 2011

MTAMBO WA GONGO NA SNAKE MAN KUPANDA ULINGONI LEO

 
Mratibu wa pambano la Ngumi za kulipwa, Shabani Adios 'Mwayamwaya' akiwa katikati ya mabondia,Maneno Osward 'Mtambo wa Gongo' kushoto na Rashidi Matumla 'Snake Man', baada ya kupima uzito leo, kwa ajili ya pambano lao, litakalofanyika kwenye Ukumbi wa Helnken Mtoni Kijichi, Dar es Salaam siku ya Xmasi. (Picha na www.superdboxingcoach.blogspot.com)
Mabondia,Maneno Osward 'Mtambo wa Gongo' kushoto na Rashidi Matumla 'Snake Man', wakipima uzito leo, kwa ajili ya pambano lao, litakalofanyika kwenye Ukumbi wa Helnken Mtoni KIjichi, Dar es Salaam siku ya Xmas

MSONDO NA SIKINDE WAKO KWENYE MPAMBANO MKALI USIKU HUU, NANI ATAIBUKA MKALI!!!?

Nani zaidi kati ya Msondo na Sikinde leo?

Na Mwandishi Wetu
Bendi kongwe nchini Msondo Ngoma Music na Mlimani Park Orchestra “Sikinde Ngoma ya Ukae”
zinatapambana leo (Krismasi) mchana hadi usiku wa manane kwenye viwanja vya TCC Club Chang'ombe jijini Dar es Salaam.
Pambano hilo ambalo tayari limevuta hisia za mashabiki wa muziki wa dansi imeandaliwa na Keen Arts na Bob Entertainment chini ya udhamini wa Konyagi.
Onyesho hilo pia ni maalum kwa ajili ya kusherehekea sikukuu ya Krisimasi ambapo wapenzi wa muziki watajumuika kwa pamoja kwenye viwanja hivyo kufurahia kumalizika kwa mwaka.
Bendi hizo ambazo zina mashabiki wengi nchini kuliko bendi nyingine zozote, zimeahidi kutowaangusha mashabiki wao kwa kila moja ikijinasimu kuwa itaibuka na ushindi.
Mara nyingi bendi hizo zikipambana huwa ni patashika nguo kuchanika, kwani mbali na mashabiki kushangilia bendi wanazozipenda vibweka na vituko kemkem vimekuwa vikitawala.
Sikinde ambayo iliweka kambi jijini Dar es Salaam imejinasibu kuibwaga Msondo na kudai kuwa hivi sasa haitishi kama ile ya miaka kadhaa iliyopita.
Itakuwa ni mara ya kwanza bendi hizo kupambana Wilayani Temeke na pia sikukuu ya Krisimasi tangu zianzishwe

MAY THE WONDEFUL BLESSING OF THIS HOLY CHRISTMAS DAY BE WITH YOU.

Krismas imeingia , Messiah kazaliwa tusherehekee kwa amani na upendo utawale kwa watu wote


Mpitanjia akipatana bei na muuzaji wa mapambo kando ya barabara ya Msimbazi, Kariakoo jijini Dar es Salaam, yakiwa ni maandalizi ya Sikukuu ya Krismasi. (Picha na Mohamed Mambo)

Alhamisi, 22 Desemba 2011

HAPPY BIRTHDAY MAMBOBADO!!!!!! BLOG YATIMIZA MWAKA MMOJA TANGU IANZISHWE, HONGERA KWA WADAU WOTE WANAOTEMBELEA HAPA KWA KUTENGENEZA JAMII YETU ILIYOSIMAMA IMARA.

Kama mtoto huzaliwa na kisha baadae kukua na kupitia hatua kadhaa za mabadiliko, basi kijiwe chetu kilianza hivyo mwaka mmoja uliopita kama sehemu binafsi ya kujifurahisha kwa mitundiko ya nyumbani na marafiki zetu, lakini baadae kikakua na kujumuisha mambo mengi ya kijamii.
Shukurani kwenu wote mliobahatika kuona kijiwe hiki kwa njia yoyote ile na kufanya wengi zaidi Duniani kote wakifahamu na kuongeza idadi ya kurasa zinazofunguliwa na kufanya jamii yetu ikue kwa kasi, wachache kati yao si vibaya nikiwataja Kamanda Phili wa Manyanya wa kule bondeni kwa Madiba, Pastor Kalu toka Mbeya, Dada Yasinta(Kapulya Mdadisi) akiwa na shemeji yetu huko Ughaibuni, Simon Kitururu Mzee wa Falsafa ndani ya Neno, Israel Saria wa BBC, Emu Three, Rehema Fussi wa Dar, Flora Talent, Michuzi mkubwa.
Huyu dogo anaitwa Omari, naye ni mdau maana huwa anapenda kushika vifaa vyangu vya kazi na kunifanya nimbembeleze aache ili niendelee na kazi, Maoni yenu ni muhimu ili kuboresha Kijiwe chetu, mwisho tumshukuru Mungu kwa kutupa uwezo wa kuendeleza mambo yetu tunayoyapenda mpaka tukafanikiwa hivi. 
Kamanda Hansom Omari akiwa katika pozi anatafakari, nimechelewa kuweka maelezo haya sababu ya shida ya umeme huku kwetu mikoa ya Lindi na Mtwara, tusameheane,tupo pamoja msijali,Tchao.

Jumatano, 21 Desemba 2011

WANASIASA WAILAUMU TAKUKURU

WANASIASA wameinyooshea vidole Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa Tanzania
(TAKUKURU), wakitaka wajisafishe ili iaminike na kurudisha heshima yake katika jamii.

Wakichangia mada iliyotolewa na Mkurugenzi wa Elimu kwa Umma kutoka Takukuru, Mary Mosha katika mafunzo ya viongozi wa Baraza la Vyama vya Siasa kuhusu Uongozi, Uwajibikaji na Utawala Bora, wanasiasa hao walisema kuwa Takukuru ni chanzo cha rushwa nchini.

Ms Mary Mosha, Mkurugenzi wa Idara ya Elimu kwa Umma Takukuru.


Akichangia mada hiyo, Katibu wa Halmashauri Kuu ya Taifa (NEC) Itikadi na Uenezi wa Chama Cha Mapinduzi, Nape Nnauye alisema kwa sasa Takukuru harufu yao mtaani siyo nzuri.


Nape alisema katika hata mambo ya kawaida yanayoonekana yana mazingira ya rushwa ikiwemo miradi ya maendeleo, maofisa wa Takukuru wamekuwa wakidai wanaendelea na uchunguzi huku wananchi wakizidi kuwalalamikia.


“Takukuru harufu yenu mtaani kwa sasa siyo nzuri, wakati mwingine inaonekana wazi mnatumika kusafisha watu, sasa itafika mahali watu wataona Takukuru ni mzigo maana wanalipwa fedha za walipa kodi, lakini kazi yao haionekani,” alisema Nape.


Alisema watu wamekuwa wakiona rushwa ni ya uchaguzi wakati kuna rushwa mbaya zaidi kwa
baadhi ya watumishi kutumia rasilimali pasipo mpangilio au kwa malengo ambayo hayakukusudiwa bila kuchukuliwa hatua zozote.


“Kwa sasa tunaona rasilimali hazitusaidii kwa sababu wanaowajibika kuzisimamia hawatimizi wajibu wao, inatupasa kila mmoja wetu kutimiza wajibu wake kwa sababu Takukuru mkiendelea hivi wananchi watawachukia sana,” aliongeza Nape.


Mwenyekiti wa Baraza hilo ambaye pia ni Mwenyekiti wa Taifa wa chama cha NLD, Dk. Emmanuel Makaidi, alisema adui mkubwa wa rushwa nchini ni Takukuru yenyewe kwa kuwa uwajibikaji wao ni mbovu na viongozi wake hawatekelezi majukumu yao ipasavyo.


Kwa upande wake, mwanasiasa mkongwe nchini, Lifa Chipaka ambaye pia ni Mwenyekiti wa Taifa wa TADEA, alisema rushwa haipo tu ndani ya vyama, bali hata ukwepaji wa kodi unaofanywa na wafanyabiashara ni rushwa.


Chipaka alisema watumishi wa Takukuru wamekuwa wakilipwa fedha nzuri, wakipewa magari ya kifahari ya kutembelea na nyumba nzuri, lakini hakuna wanachokifanya katika jamii.


Mapema, akitoa mada yake, Mosha alisema kama vyama vya siasa visipodhibiti rushwa ndani ya vyama vyao, vitashindwa kudhibiti hata nje ya vyama na hivyo kusababisha kupatikana viongozi wasiofaa.

NEWS ALERT!!!!!! JIJI LA DAR LAKUMBWA NA MAFURIKO MABAYA ASUBUHI HII, MAGARI YA SAFARI ZA MIKOANI YAKWAMA HUKO MBEZI BAADA YA DARAJA MOJA KUFURIKA MAJI HADI JUU YA NJIA, MABIBO RELINI HAKUPITIKI, MAGARI YASOMBWA,WANANCHI WACHUKUE TAHADHARI.

Wananchi wa eneo la Jangwani Dar es salaam wakiwa barabarani wakikimbia nyumba zao ambazo ziliingiliwa na mafuriko ya maji jana kutokana na mvua zinazonyesha kuanzia jana hadi leo, maafa ni makubwa

Wananchi wa Jangwani Magomeni wakijaribu kuokoa baadhi ya vifaa baada ya mafuriko kuzidi, pembeni kuna mkokoteni uliosheheni taka na kutelekezwa hapo, Idara ya Afya ijidhatiti kwa lolote maana magonjwa ya mlipuka yanaweza kutokea, poleni sana.
(Picha kwa hisani ya issamichuzi blog)

PICHA ZAIDI
Eneo la Jangwani
Gari ya Zimamoto bila kujua ilipita kwenye barabara iliyojaa maji kumbe daraja limekatika.
Harakati za uokoaji.
Jangwani haifai tena na si eneo salama la kuishi, poleni waathirika wote.

Jumanne, 20 Desemba 2011

BAADHI YA WANANCHI WALAUMU KAFULILA KUFUKUZWA UANACHAMA NCCR

Mh. D. Kafulila


Mbunge huyo alionekana anastahili adhabu hiyo baada ya kupitia tuhuma nzito zilizotolewa juu ya Mwenyekiti wa chama hicho, James Mbatia
Wajumbe walipokea na kujadili kina na kura zikapigwa na kuonekana mbunge huyo kutokuwa na imani na mwenyekiti wake na kwenda kinyume na taratibu za chama hicho.

Mbali na kuvuliwa uanachama kwa mbunge huyo pia Hashim Rungwe aliyewahi kuwa mgombea urais katika Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2010 nae amevuliwa uanachama.
Hivyo kwa kuvuliwa uanachama kwa mbunge huyo kwa mujibu wa sheria jimbo hilo litakabiliwa na uchaguzi mdogo kupatikana kwa mbunge

Kufuatia sakata hilo, msajili wa Vyama vya Siasa nchini, John Tendwa amelaani vikali na kukitupia lawama chama hicho kwa kitendo cha kumvua uanachama mbunge huyo na kuita kitendo hicho ni cha kukomoana na kusababisha gharama zisizo za lazima kwa Taifa kugharamia Uchaguzi Mdogo katika jimbo hilo

Kwa upande wa Chama cha Chadema kimemkaribisha mbunge huyo kijana machachari kujiunga na chama hicho baada ya kufukuzwa NCCR-Mageuzi.
"Milango yetu ipo wazi kwa mujibu wa Katiba, Kanuni na taratibu za chama chetu,"kilisema chama hicho

Hata hivyo baadhi ya wananchi nao walilaani kitendo hicho cha kumvua uanachama mbunge huyo ambaye alikubalika jimboni kwake kuokana na harakati zake za kutetea wanaanchi wa jimbo lake na kitendo hicho kimeonekana na sawa na kuwanyanyasa wananchi wa jimbo hilo

Jumapili, 18 Desemba 2011

RAIS ANAYETUHUMIWA NA ICC AHAIRISHA ZIARA YAKE TANZANIA.

 
Picture
Tanzania's President, Jakaya Kikwete (L) speaks during a joint press conference with his Sudanese counterpart Omar al-Bashir (R) in Khartoum on September 8, 2008 (library photo: AFP)
The Sudanese president Omer Hassan al-Bashir has reportedly cancelled a trip he was planning to make to Tanzania last week.

Local newspapers in Khartoum said that Bashir was headed to Dar es Salaam on Friday December 9th for talks with his Tanzanian counterpart Jakaya Kikwete on issues of mutual concern. He was to be accompanied by his foreign Minister Ali Karti, Defence Minister Abdel-Rahim Mohamed Hussein and minister of the presidency Bakri Hassan Saleh.

Tanzania along with Uganda has recently voted against Sudan’s bid to join the East African Community (EAC) citing concerns over Khartoum’s democratic practices and its treatment of women as well as geographic proximity.

Bashir was apparently planning to participate in the celebrations marking Tanzania’s 50th Independence Day which took place last Friday.

But the visit was called off last minute for coinciding with swearing in ceremony of new cabinet and was to be rescheduled.

This would have been the fifth country visited by the Sudanese leader that is a member of the International Criminal Court (ICC).

Bashir is the first sitting president indicted by the ICC, which issued an arrest warrant on charges of genocide, crimes against humanity and war crimes in Sudan’s troubled Darfur region.

source: http://www.wavuti.com/

AVUNJA REKODI YA MSICHANA MFUPI KULIKO WOTE DUNIANI.

Msichana mfupi kuliko wote duniani


NewsImages/6129114.jpg
Bibie Jyoti Amge akichukuliwa vipimo vya urefu wake.
Mwanafunzi wa Kihindi, Jyoti Amge, ni msichana aliyevunja rekodi ya dunia ya msichana mfupi kuliko wote duniani, kwa mujibu wa rekodi inayosajiliwa na kitabu cha rekodi cha Guinness.
Runinga ya NBC ya Marekani, siku ya Ijumaa 17/12/2011, imeripoti kuwa Jyoti Amge mwenye umri wa miaka kumi na minane 18, ana urefu wa sentimeta 62.8. sawa na inchi 24.7. Kwa hiyo msichana huyo ndio msichana mfupi kuliko wote duniani akiwa amempita msichana wa Kimarekani Bridgette Jordan mwenye umri wa miaka ishirini na miwili 22, ambaye ana urefu unaovuka ule wa Jyoti Amge kwa sentimeta saba 7. Kwa mujibu wa habari hiyo, Bridgette Jordan, alikuwa anashikilia rekodi hiyo tangu Septemba 2011.

Siku ya Ijumaa, Bibi Jyoti Amge, alikuwa anasherehekea siku yake ya kuzaliwa katika jiji la Nagpur. Wakati huo huo amenukuliwa akisema “Furaha ilioje kwa kusherehekea siku yangu ya kuzaliwa kwa kutimiza miaka kumi na minane 18 nikishika rekodi mpya. Kwa kweli tukio hili ni zawadi ya nyongeza kwa sherehe ya kuzaliwa kwangu.”

BARCELONA YATWAA UBINGWA WA VILABU DUNIANI, WAICHAPA SANTOS YA BRAZIL

Barcelona wameshinda kombe la dunia la Fifa kwa vilabu baada ya kuicharaza timu ya Santos ya Brazil kwa mabao 4-0 kwenye mchezo wa fainali uliyochezwa nchini Japan.
Barcelona mabingwa wa kandanda kwa vilabu duniani
Barcelona mabingwa wa kandanda kwa vilabu duniani


Ushindi huo umeendeleza rekodi nzuri ya klabu hiyo kwa mwaka huu ambapo wao ni mabingwa wa Ligi ya Hispania maarufu La Liga, wanashikilia ubingwa wa vilabu vya Ulaya na pia Kombe la Hispania maarufu Spanish Super Cup.
Mpachika mabao wa timu ya taifa ya Argentina Lionel Messi alifunga mabao mawili, huku mengine yakiwekwa kimiani na Xavi pamoja na nahodha na kiungo wa zamani wa Arsenal Cesc Fabregas.
Ushindi huo unathibitisha kwamba Barcelona inaendelea kusalia timu bora ya kusakata kandanda duniani.
"Tulicheza mchezo wetu kwa ukamilifu," alisema nahodha Carles Puyol. "Ulikuwa mchezo mzuri, mchezo mgumu sana na tumefurahi sana kwa matokeo haya."
Mchezo huo baina ya mabingwa wa kandanda wa Ulaya na wa Amerika Kusini mjini Yokohama ulikuwa ukitajwa kuwa kivutio kati ya Messi, anayeaminika ndiye mchezaji bora wa soka duniani na mshambuliaji hatari wa Brazil mwenye umri wa miaka 19 Neymar, ambaye anatajwatajwa huenda akajiunga na ama na Barca au Real Madrid.
Lakini haikuwa hivyo - Messi akionekana kushamiri katika mchezo huo na kutajwa mchezaji bora wa mechi hiyo na pia akapata tuzo ya mchezaji mwenye thamani kubwa katika michuano hiyo wakati Barcelena ikiweka kibindoni kombe la ubingwa wa dunia kwa mara ya pili mfululizo katika misimu mitatu.
Bao lake la kwanza alifunga kwa kuubetua mpira kama ilivyo kawaida yake na la pili alifunga kwa ustadi mkubwa baada ya kumzunguka mlinda mlango wa Santos Cabral.
Santos walibadilika na kucheza soka nzuri kipindi cha pili na Neymar nusura afunge baada ya kupatiwa pasi nzuri akiwa amebakia peke yake na mlinda mlando wa Barcelona Victor Valdes, lakini Valdes akafanikiwa kuokoa.
"Barcelona walistahili kushinda. Ni timu bora duniani na tumejifunza somo muhimu," alisema Neymar.
Timu ya Qatar ya Al Sadd, ambayo ililazwa mabao 4-0 na Barcelona katika hatua ya nusu fainali, iliwafunga mabingwa wa Japan Kashiwa Reysol mabao 5-3 kwa mikwaju ya penalti na kufanikiwa kushika nafasi ya tatu ya michuano hiyo inayofanyika kila mwaka kwa kushirikisha mabingwa wa soka wa mabara duniani

Ijumaa, 16 Desemba 2011

CUF NA NCCR MMEPATWA NA NINI!!?



Mbunge wa Wawi, Hamad Rashid Mohamed

Waandishi Wetu
WAKATI uongozi wa CUF, ukiwa bado haujamwita kwenye Kamati ya Maadili, Mbunge  wa Wawi, Hamad Rashid Mohamed, Mbunge wa Kigoma Kusini, David Kafulila, amesema hatishwi na kikao cha dharura cha Halmashauri Kuu ya chama chake cha NCCR-Mageuzi, kinachotarajiwa kuketi kesho kumjadili kama inavyodaiwa.
CUF na NCCR- Mageuzi vimekuwa katika migogoro ya ndani kwa muda mrefu na kadiri siku zinavyosonga mbele, migogoro hiyo inaonekana kuendelea kukua kiasi cha kutishia uhai wa vyama hivyo vya upanzani.
Upande wa CUF
Wakati uongozi wa chama hicho ukiwa bado unasuasua kumpa barua ya wito Hamad kama ilivyoahidiwa na Naibu Katibu Mkuu wake Bara, Julius Mtatiro, wanachama 4,000 wa chama hicho Kata ya Manzese, jijini Dar es Salaam wameonya kwamba kitendo cha kumzuia mbunge huyo kufanya mikutano, kinaweza kusababisha mpasuko mkubwa ndani ya chama.
Mtatiro jana aliliambia gazeti hili kuwa chama hicho bado hakijampekelea barua Hamad  kumwita kwenye kikao hicho cha maadili, lakini mpango wake huo, haujabadilika.
"Bado tutampelekea tu na tutamuita  katika Kamati ya Maadili ya chama muda wowote  kuanzia sasa,”alisema Mtatiro.
Akieleza sababu za kumwita mbunge huyo pekee na sio Maalim Seif Sharif Hamad, Mtatiro alisema Hamad Rashid, ndiye aliyeanza kuzungumza na waandishi wa habari na kueleza matatizo yake aliyonayo ndiyo maana uongozi ukabaini kwamba kuna kila sababu za kumuita na kuzungumza naye.
Alisema baada ya kumwandikia barua,  vikao vya ndani vya chama vitakaa na kumhoji na maamuzi yatakayotafanyika kikatiba ndio yatakayoamua hatima yake. “Vikao vya ndani ndivyo hasa vitakavyojua  hatma ya Hamad Rashid na sio mimi. Kwa kweli siwezi kukueleza chochote kile sasa hivi,”alisema
Wakati chama kikipanga kumwita, Hamadi mwenyewe amezungumzia hatua hiyo kuwa ni ukiukwaji mkubwa wa katiba akieleza kuwa kimsingi alipaswa kuitwa katika vikao vya chama na sio kuhukumiwa na kushutumiwa kupitia vyombo vya habari.
Kauli ya mbunge huyo wa Wawi ilikuja baada ya Mtatiro kutoa kauli kwenye mkutano na wanahabari akidai kuwa kitendo cha Hamad kufanya mkutano na wanachama wa Tawi la Chechinya, Manzese  bila kibali  cha chama ni kwenda kinyume na taratibu.
Wananchama 4,000
Wakati uongozi huo  wa CUF ukisuasua kumpa barua Hamad wanachama 4,000 wa Kata ya Manzese jijini Dar es Salaam, wameonya kuhusu kitendo cha kumzuia mbunge huyo kuendelea na mikutano yake.
Wanachama hao waliyasema hayo jana kufuatia mbunge huyo kushindwa kukabidhi msaada wa samani za ofisi ya kata hiyo alizopaswa kuzikabidhi Desemba 11 mwaka huu, lakini akazuiwa na ulinzi wa chama hicho wanaojulikana kama Blue Guard.
Katibu wa Kata hiyo, Hamdan Kulangwa alisema kitendo cha mbunge huyo kuzuiwa na walinzi wa chama hicho kinakiuka taratibu za chama na hivyo kuwasikitisha sana wapenzi na wanachama wake katika kata hiyo.
“Sisi tulimwalika Hamad Rashid aje atukabidhi msaada wa samani za ofisi ambazo tulimwomba atusaidie, lakini siku ya tarehe 11 Disemba, alipofika kabla hajaanza kufanya lolote lilikuja kundi la Blue Guard na kumzuia kuzungumza na sisi,” alisema Kulangwa
Kafulila: Sina hofu kikao cha NEC
Wakati upepo ukivuma vibaya ndani ya CUF, NCCR nako mambo bado magumu baada ya mbunge wa Kigoma Kusini, David Kafulila, kusema kuwa hana hofu na kikao cha NEC ya chama hicho inayoketi  kesho.
Kafulila ambaye anadaiwa kuzungumza mambo ya ndani ya chama katika vyombo vya habari pamoja na kupingana wazi wazi na mwenyekiti wake, James Mbatia kinyume alisema  hana wasiwasi kwa kuwa mpaka sasa hakuna ajenda zilizowekwa wazi juu ya mambo yatakayojadiliwa katika kikao hicho.
Kafulila alisema, “Mimi ni mjumbe wa kikao hicho na nitakuwepo, ila mpaka sasa sijaelezwa ajenda…, hili ni jambo dogo na kila kitu kitajulikana katika kikao, nadhani kikao kitajadili mambo mbalimbali,” alisema Kafulila.
Alipoulizwa hoja atakazoziwasilisha iwapo atajadiliwa katika kikao hicho, Kafulila alisisitiza kwamba hawezi kulizungumzia suala hilo kwa kuwa mpaka sasa hajui nini kitakachojadiliwa.


Imeandaliwa Fidelis Butahe, Hussein Issa na Aidan Mhando

Jumatano, 14 Desemba 2011

JAN POULSEN AIPASHA TFF


Sweetbert Lukonge
KOCHA wa timu ya Tanzania, Jan Poulsen amelishutumu waziwazi Shirikishi la Soka nchini (TFF) kwa kuharibu mipango yake ya maandalizi ya mechi za kufuzu Kombe la Dunia 2014.Poulsen aliondolewa kuifundisha timu ya taifa ya Tanzania Bara 'Kilimanjaro Stars' kwenye mashindano ya Kombe la Chalenji yaliyomalizika hivi karibuni na Uganda kuibuka mabingwa.


Nafasi hiyo ya Poulsen walipewa makocha Charles Mkwasa na Jamhuri Kiwehlu ikiwa na wachezaji wa Tanzania Bara pekee kwa sababu Zanzibar nayo inashiriki michuano hiyo.


"Kazi yangu inakuwa ngumu sana kwa sababu tunatakiwa kujipanga kwa ajili ya mechi zetu za kufuzu 2012," Poulsen aliimbia BBC."Napopata fursa ya kuwa na wachezaji kwa muda mrefu ndivyo ninavyowafahamu zaidi. Muda uliobaki ni mfupi kabla ya kuanza kwa mechi za mchujo hapo Juni.


"Unaweza ukajiuliza kuna umuhimu gani wa kubadilisha timu kwa kiasi kubwa kwa ajili ya michuano ya Chalenji badala ya kuendelea kuwa na kikosi kile kile kilichocheza mechi mbili za mwisho dhidi ya Chad," alisema Poulsen.


Mdenmark huyo alikuwa kwenye jukwaa wakati Kilimanjaro Stars ikitupwa nje kwenye nusu fainali na Uganda na kuzomewa na mashabiki wake.Alipoulizwa kama ilikuwa na umuhimu wote kwa makocha hao ndani kuifundisha timu hiyo, Poulsen alisema.


"Sina uhakika kama ningeweza kufanya hivyo mimi. Lakini TFF wana sababu zao na jinsi wanavyotaka kuendeleza soka la Tanzania," alisema."Nafikiri tunatakiwa kujipanga kwa umakini na kuwa na mawasiliano mazuri kati yetu. Ni matumaini yangu mambo yatakuwa mazuri siku zijazo."


Akijibu madai hayo ya Poulsen, katibu mkuu wa TFF, Angatile Osiah alisema uamuzi huo ulitokana na kilio cha Watanzania wengi kutaka kocha asiifundishe Kilimanjaro Stars.


"Yeye ni kocha mkuu wa timu ya Taifa ya Tanzania na sio Tanzania Bara (Kilimanjaro Stars)," alisema Osiah.

SHILINGI BILIONI 64 ZATUMIKA KUGHARAMIA SHEREHE ZA MIAKA 50 YA UHURU WA TANGANYIKA.


The government of Tanzania spent a total of TSh. 64 billion  to facilitate celebrations to mark the  50th independence anniversary of  Mainland Tanzania.

Sources from the celebrations organising committee and Treasury confided separately to The Citizen that the  money was  spent on exhibitions by all ministries and some government agencies, plus the grand gala that marked the  climax  of the event  at Uhuru Stadium in Dar es Salaam last Friday.

Some Sh8 billion was allocated to local governments. Regional administration and local government authorities organised celebrations in  all  of the Mainland’s 21 regions, and 136 district councils.

Major  items on which the money  was spent included preparatory logistics, fuel, per diem for civil servants and printing costs for leaflets highlighting  achievements that   respective districts and regions had registered over the 50-year period.In Dar es Salaam, the celebrations started in earnest in July, shortly after the Public Service Week. Ministries took turns  at the Mnazi Mmoja grounds, to showcase their  activities.

Ministerial exhibitions, per diem dues ‘ and other exhibition-related expenses ‘swallowed’ between Sh9 and 11 billion, the source from Treasury hinted.

The same source revealed that about Sh213 million was given to Tanzania trade Development Authority (TanTrade), to finance some ministerial  exhibitions as well as those of state agencies and  the private sector, at Mwalimu Nyerere exhibition grounds along Kilwa Road in Dar es Salaam.

Reached for comment last week, the TanTrade chief executive officer, Mr Ramadhan Khalfan, said his organisation  had presented  a budget of Sh613 million  for the exhibitions but was given only Sh213 million.He also said the government barred them from charging entry fees to recoup some of the expenses incurred in organising the fair.

“Our budget was for preparations of the pavilions to enable the exhibitors to have a convenient  area and space to showcase their activities... we are not part of other expenses on the Uhuru exhibitions held elsewhere,” Mr Khalfan said.

Some reports  suggest that money  wasn’t allocated equitably to ministries, citing Sh600million  for the Ministry for Finance and Economic Affairs  for the 12-day exhibition at Mwalimu Nyerere grounds.A senior officer within the Finance ministry who is also part of the team at the exhibition that ends today, said  staff manning the pavilion are paid  a daily  Sh100,000 allowance  each.

Enquiries by this paper showed that allocations to ministries ranged from Sh30million to Sh150 million.  The ministry of Industries, Trade and Marketing reportedly received Sh30million. Each of the nearly 5,000 youngsters who participated in the mass display on Friday  was reportedly paid Sh40,000, but a figure for defence and security staff who staged  various shows couldn’t be obtained
.
Credits; The Citizen

BADO UTATA WAGUBIKA KIFO CHA KONSTEBO DAVID ALIYEJIUA LINDONI NMB.

Askari Polisi wakijaribu kuwatawanya wananchi waliokuja kushuhudia tukio hilo la askari kujiua nje ya Makao Makuu ya Benki ya NMB mtaa wa Azikiwe na Jamuhuri.

ASKARI Polisi, Konstebo David Selemani (22) aliyejiua kwa kujipiga risasi jijini Dar es Salaam inadaiwa kabla ya kuchukua uamuzi huo, aliwasiliana na ndugu zake wengi wakiwemo ambao hakuwa amewasiliana nao kwa muda mrefu.


Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Ilala, Faustine Shilogile ambaye kwa mujibu wake polisi inaendelea na uchunguzi kubaini sababu za kufanya hivyo, alisema hatua hiyo iliwashangaza ndugu hao.


Shilogile alisema uchunguzi unaofanyika ni pamoja na kuwasiliana na kampuni ya simu ya mtandao aliokuwa akiutumia ili kufahamu mtu aliyekuwa akiwasiliana naye kabla ya kujiua.


Kwa upande wa ndugu na marafiki wa askari huyo waliozungumza na gazeti hili kabla ya mwili wake kusafirishwa kwenda mkoani Kilimanjaro kwa maziko, walisema wanaendelea kujiuliza maswali bila majibu juu ya sababu za jamaa yao kuchukua uamuzi huo.


Katika kuaga mwili wa Konstebo David katika Hospitali ya Taifa Muhimbili, mmoja wa ndugu aliyejitambulisha kwa jina moja la Danny, alisema siku moja kabla ya kujiua, alizungumza naye kwa simu akimtaka waonane.


“Mimi shughuli yangu ni dereva, na kwa bahati mbaya siku hiyo nilikuwa safarini, hivyo nilimtaka wakaonane na kaka yangu ili wazungumze kama kulikuwa na jambo la haraka la kuzungumza, sababu nilijua lingeweza kupatiwa majibu na kaka,” alisema Danny.


Alisema siku iliyofuata, akiwa njiani kurudi Dar es Salaam, alishitushwa kupata taarifa za msiba wa David, suala alilodai kuwa limemuacha na maswali mengi juu ya kile kilichosababisha ajiue.

Jumamosi, 10 Desemba 2011

THIERY HENRY AKUMBUKWA KAMA SHUJAA WA ASERNAL KWA KUCHONGEWA SANAMU NJE YA UWANJA WA IMARATI.

Teary Henry as Arsenal unveil statues to former French star, Adams and Chapman

Thierry Henry paid an emotional tribute to Arsenal and his former team-mates after seeing himself immortalised in a bronze statue outside Emirates Stadium on Friday afternoon.
The Gunners record goalscorer was one of three club legends to be honoured as part of their 125th anniversary celebrations, with former manager Herbert Chapman and also captain Tony Adams, who led Arsene Wenger's men to the Double twice, each receiving a similar tribute.
Henry left Arsenal for Barcelona in June 2007, where the Frenchman would go on to lift the Champions League before moving to the Major Soccer League in the United States with New York Red Bulls.
Emotional: It's all a bit much for Thierry Henry as his statue is unveiled
Emotional: It's all a bit much for Thierry Henry as his statue is unveiled
Icon: Arsenal's tribute to former striker Henry
Icon: Arsenal's tribute to former striker Henry
How it should look: Henry celebrating his goal against Spurs back in the 2002/03 season
How it should look: Henry celebrating his goal against Spurs back in the 2002/03 season
The 34-year-old, however, insists Arsenal will always remain in his heart.
'I never thought in my wildest dreams that I would have a statue like this in front of the stadium of the team I love and support,' said Henry, who netted 226 goals as the Gunners won two Premier League titles and the FA Cup twice.
'The way the statue is gives the perfect example of the love I have for the club - me kneeling facing the Emirates Stadium and Highbury behind is amazing.
'I also have to thank the fans, you have always been special, and I always try to give my best, I know times it was not enough, but I always give it all out there on the field for you guys and the club.
'It is kind of weird to think of the amount of great players who have played for Arsenal, and for me to be right here, I have to say thanks to all of them, because I would not be able to be right there kneeling in front of this stadium, without them.
'Also, I must give a special thanks to my close friends.....'
Solid: Tony Adams has a permanent place outside the Emirates Stadium
Solid: Tony Adams has a permanent place outside the Emirates Stadium
After taking a few moments to compose himself, Henry added: 'I know some of the press used to kill me for not showing emotion - well, there you go, I am showing emotion for the club I love.
'Whatever I do, I do it with my heart, that is the way I am.
'It was not always easy to cope with the pressure of delivering, but from the bottom of my heart, I want to thank Arsenal Football Club for giving me this opportunity to be here in front of this club I love - once a Gooner, always a Gooner.
'Thank you from the bottom of my heart, but I played with some great players too and it would not have been possible without them.'
Standing proud: The statue of Herbert Chapman
Standing proud: The statue of Herbert Chapman
Gunners boss Wenger had worked with Henry during their time at Monaco, and was instrumental in helping mould the French winger into one of the world's best players following his £11million move from Juventus in the summer of 1999.
Wenger hailed his former captain as the model professional.
'Thierry deserves the honour he gets today, and I am very proud to witness it,' the Gunners boss said.

'His sensational career was down simply to Thierry's class. He is a player who had everything you dream of as a manager - physical potential, a technical level, super intelligence and what people also forget for many top level athletes, is he was dedicated to his job, with a very serious life.
'He is simply a model (professional) who won everything you can in our world - Thierry, you were really special


Read more: http://www.dailymail.co.uk/sport/football/article-2072146/Arsenal-statues-unveiled-Thierry-Henry-tears.html#ixzz1g7jMyfIE

JESHI LA WANANCHI WA TANZANIA LASHIRIKI KUADHIMISHA MIAKA HAMSINI YA UHURU WA TANGANYIKA.

MIAKA 50 YA UHURU WA TANZANIA ILIVYOADHIMISHWA NA JESHI LA WANANCHI (JWTZ)

Mara baada ya Amiri Jeshi Mkuu Rais Dk. Jakaya Kikwete kukagua vikosi vya ulinzi na usalama na vikosi hivyo kutoa heshima kwa Amiri Jeshi Mkuu huyo, kwenye maadhimisho ya miaka 50 ya Uhuru wa Tanzania leo katika uwanja wa Uhuru, yalifuatia maonyesho ya vifaa vya kijeshi vilivyoonyeshwa na jeshi tukufu la Tanzania JWTZ, ambapo askari wa jeshi hilo wakiwa wakakamavu, walipita na kuonyesha vifaa vya kivita kama linavyoonekana na gari hili ni la Rada hutumiwa na jeshi la wanamaji likiwa na
Haya ni Magari maalumu yanayotumiwa na wanajeshi wa majini kama yanavyoonekana.
Haya ni magari ya kulinda amani katika programu za umoja wa mataifa.
haya ni magari ya makombora ya masafa marefu.
Vifaru vinavyopiga masafa marefu.
Vifaru vya Doria
Magari haya maalum pia ni kwa ajili ya Doria
Hili ni gari maalum kwa ajili ya madaraja
Hili ni gari lililotengenezwa na kiwanda cha Nyumbu kinachomilikiwa na JWTZ.
Hili ni gari lililotengenezwa na kiwanda cha Nyumbu kinachomilikiwa na JWTZ ambalo kazi yake kubeba mizigo.
Credits; Fullshangwe