Jumanne, 31 Mei 2011

DAKTARI POSTMOTERM YA TARIME ATISHIWA MAISHA.

Mauaji Tarime: Daktari atishiwa kuuawa  Send to a friend
Anthony Mayunga, Tarime
DAKTARI aliyesimamia uchunguzi wa miili ya watu wanne kati ya watano waliouawa na Polisi Mei 16, mwaka huu akiziwakilisha familia za wafiwa amedai kwamba ametumiwa ujumbe wa maandishi kwa simu kwamba atauawa.

Daktari huyo, Grayson Nyakarungu wa Mwanza alisimamia uchunguzi wa miili ya Chacha Ngoka, Emmanuel Magige, Bhoke Chawali na Mwikwabe Mwita katyika uchunguzi uliofanyika Mei 23, mwaka huu.

Alisema kwamba alipokea ujumbe wa simu mara mbili kwa nyakati tofauti Mei 26, mwaka huu akiwa safarini kuelekea Dar es Salaam uliojaa vitisho.

Alidai kwamba moja wa ujumbe huo unaosomeka, “Hizo ripoti siyo za kisiasa, acha kujiingiza kichwa kichwa utajutia, Tundu Lissu ndiye anakutumia ili yeye apate umaarufu, usipokoma kwa onyo hili, tutakushughulikia, subiri mahakamani ukatoe ushahidi, usidanganywe...”

Dk Nyakarungu alisema mara baada ya kupokea ujumbe huo, alipiga simu katika namba hiyo na kupokewa na mwanamke aliyedai kuwa yuko Mwanza ambaye hakutaka kujitambulisha. Alidai kwamba mara baada ya kukata simu hiyo, alipokea ujumbe mwingine uliosema:

“Hata ukitutambua utafanya nini, narudia mara ya mwisho, hizo ripoti haziwahusu wanahabari, funga domo lako.”Dk Nyakarungu alisema kwamba ametoa taarifa juu ya matukio hayo katika Kituo cha Polisi, Oystebay, Dar es Salaam na kufunguliwa jalada namba OB/RB/9214/11.

Hata hivyo, alisema licha ya vitisho hivyo hataogopa kwa kuwa alitumwa na familia na amelazimika kuwapa taarifa zote zilizojitokeza.Alisema inaelekea kuwa aliyetuma ujumbe huo amekuwa akimfuatilia kwa kuwa ametuma ujumbe huo katika namba zake mbili tofauti za simu.

ZUMA AJITOSA KUMALIZA MGOGORO WA LIBYA.

Zuma kujaribu kutatua mzozo wa Libya

Jacob Zuma
Jacob Zuma
Rais wa Afrika Kusini Jacob Zuma amewasili mjini Tripoli kwa kile kinachoonekana kuwa juhudi za mwisho za kujaribu kutafuta suluhu ya kidiplomasia ya mzozo unaoendelea.
Haifahamiki kama ziara hiyo ambayo ni ya pili kwa Bw Zuma, itaangazia kumshawishi Kanali Muammar Gaddafi kuondoka madarakani.
Waasi wanaopigana na majeshi ya Gaddafi tangu mwezi Februari wamekataa kufanya mazungumzo hadi pale atakapoondoka kwenye uongozi.
Wakati huo huo chama cha Bwana Zuma cha African National Congress kimeshutumu mashambulio ya majeshi ya Nato mjini Libya.
"Tunaungana na bara hili na watu wote wanaopenda amani duniani katika kushtumu mashambulio ya anga yanayoendelea Libya yakifanywa na vikosi vya magharibi," chama cha ANC kimesema katika taarifa siku moja kabla ya ziara ya Zuma.
Shinikizo kutoka kwa jamii ya kimataifa zinaendelea dhidi ya Kanali Gaddafi, huku nchi zinazounda kundi la G8 zikitoa wito siku ya Ijumaa ya kumtaka aondoke na rais wa Urusi Dmitry Medvedev akisema siku ya Jumamosi kwamba hana tena haki ya kuwaongoza watu wa Libya.
Waasi wa Libya waliridhishwa na taarifa hiyo ya kundi la G8.
"Dunia nzima imekubaliana kwamba Kanali Gaddafi na utawala wake hawakupoteza tu uhalali wa kuongoza lakini pia heshima," alisema kiongozi wa waasi Mustafa Abdul Jalil katika taarifa

PICHA YA LEO; ELIMU NI UFUNGUO WA MAISHA, HILO HALINA UBISHI.



Elimu popote pale, nyoka akidondoka mapumziko, mvua ikinyesha tunafunga shule.