Jumamosi, 29 Septemba 2012

MAREHEMU KAMAZIMA AMEAGWA LEO HUKO TEGETA DAR ES SALAAM TAYARI KWA MAZISHI MARUKU BUKOBA.

 

Marehemu Anatoly Kamazima(katikati) wakati alipoapishwa kuwa Wakili wa Mahakama Kuu June 2011 Dar es salaam akiwa na mawakili wenzie Joseph Kiula wa pili toka kulia na Mzalendo wa kwanza kulia, kushoto ni wakili Burhan Othman.
HISTORIA FUPI YA MAREHEMU MEJA JENERALI MSTAAFU ANATOLY KAMAZIMA.Marehemu alizaliwa mwaka 1946 katika kijiji cha Maruku, Mkoani Kagera. Alijiunga na Jeshi mwaka 1967, mara baada ya kuhitimu Chuo Kikuu mwaka 1966.

Marehemu Kamazima amesoma kozi mbalimbali za kijeshi hapa nchini na nchi za China, India, Uingereza na Misri na kulitumikia Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) katika ngazi mbalimbali ambapo mwaka 1989, aliteuliwa kuwa Mkurugenzi wa Tume ya Kuzuia Rushwa Tanzania, hadi alipostaafu Juni 2003.

Rais amemuelezea marehemu Kamazima kama mzalendo na mtu aliyeipenda na kuitumikia nchi yake kwa weledi mkubwa, uaminifu na moyo mmoja.

“Nimemfahamu Marehemu kwa miaka yote ya utumishi wake jeshini na serikalini kama mzalendo, muaminifu na mwenye moyo wa kulinda nchi yake wakati wote” amesema Rais “Marehemu Kamazima alikua mtu wa kutumainiwa sana katika nchi yetu na kamwe hatutamsahau kwa utumishi wake uliotukuka”.

“Tutamkumbuka na kumuenzi siku zote, tunamshukuru Mwenyezi Mungu kwa yote na tunamuombea mapumziko mema Marehemu Kamazima. Amina”. Rais ameongeza.

Marehemu ameacha mjane, watoto na wajukuu.

Imetolewa na:

Premi Kibanga,
Mwandishi wa Habari wa Rais, Msaidizi,
Ikulu.
DAR ES SALAAM

26 Septemba, 2012
 *************************************************************************
 Rais na Amiri Jeshi Mkuu Dkt Jakaya Mrisho Kikwete akitoa pole kwa mjane na ndugu wa wa Meja Jenerali Mstaafu Anatoli Kamazima leo nyumbani kwa marehemu Tegeta, Dar es salaam. Marehemu Kamazima, ambaye amefariki dunia usiku wa kuamkia  Jumatano ya Tarehe 26 Septemba, 2012 utokana na mshtuko wa moyo, alikuwa Mkurugenzi Mkuu wa kwanza wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa nchini TAKUKURU.


Rais na Amiri Jeshi Mkuu Dkt Jakaya Mrisho Kikwete akiongea na Brigedia Jenerali Mstaafu Tindamanyire, ndugu wa hayati Meja Jenerali Mstaafu Anatoli Kamazima, leo nyumbani kwa marehemu Tegeta, Dar es salaam. Kulia kwa Rais ni Mkuu wa Majeshi Jenerali Davis Mwamunyange na Mnadhimu Mkuu Luteni Jenerali Samwel Albert Ndomba. Marehemu Kamazima, ambaye amefariki dunia usiku wa kuamkia  Jumatano ya Tarehe 26 Septemba, 2012 kutokana na mshtuko wa moyo, alikuwa Mkurugenzi Mkuu wa kwanza wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa nchini TAKUKURU

JALADA KESI YA VIGOGO JKT LIPO KWA DPP.

James Magai
JALADA la kesi ya maofisa wa Jeshi la Kujenga Taifa (JKT) wanaokabiliwa na mashtaka ya matumizi mabaya ya ofisi za umma, limekwama kwa Mkurugenzi wa Mashtaka.Kesi dhidi ya maofisa hao saba waandamizi wa JKT, iko katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, jijini Dar es Salaam.
Mkurugenzi wa SUMA JKT ambaye ni mmoja wa washtakiwa Kanali Ayoub Mwakang'ata kulia mwenye suti nyeupe.

Maofisa hao ni pamoja na Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Uzalishaji Mali la jeshi hilo (Suma JKT), Kanali  Ayoub Emu Mwakang’ata na Mkuu wa Miradi, Luten Kanali Felix Andrew Samillani.
Wengine ni  Luteni Kanali Mkochi Chacha Kichogo, Luteni Kanali Paul Andrew Mayavi , Meja Peter Mabulla Lushika, Sajenti John Andrew Laizer na Meja Yohana Leonard Nyuchi.
Kesi hiyo ilitarajiwa kuanza kusikilizwa jana, katika hatua za awali ambapo washtakiwa wangesomewa maelezo kuhusu mashtaka yanayowakabili.

Hata hivyo ilikwama kutokana na kutokuwapo kwa jalada lao mahakamani.
Mwendesha Mashtaka wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru), Tabu Mzee, alidai kuwa jala la kesi hiyo bado liko kwa DPP, na akaomba mahakama ipange tarehe nyingine ya kuwasomea washtakiwa maelezo ya awali.

Hakimu Aloyce Katemana alikubaliana na ombi hilo na kupanga maelezo hayo yasomwe  Oktoba 26 mwaka huu.
Hii ni mara ya pili kwa vigogo hao wa JKT kushindwa kusomewa mashtaka kutokana na jalada la kesi yao kuitwa na DPP.
Awali, mahakama ilipanga washtakiwa hao wasomewe maelezo hayo  Agosti 30 mwaka huu, lakini ilishindikana kutokana na jalada la kesi kuitishwa na DPP.

Hatua hiyo ilimlazimisha mwendesha mashtaka huyo wa Takukuru kuomba kesi ipangiwe nyingine na mahakama ikapanga jana.

Washtakiwa hao walipandishwa kizimbani  Julai 2 mwaka huu na kusomewa mashtaka saba yakiwemo ya kula njama na kuhamisha zaidi ya Sh3 bilioni kinyume cha sheria.

Mwendesha Mashtaka wa Takukuru, Donasian Kessy akisaidiana na Ben Lincoln, alida kuwa washtakiwa walitenda makosa hayo kwa nyakati tofauti.
Kessy alidai kuwa walitenda makosa hayo wakati wakipitisha uamuzi wa ununuzi wa magari na vifaa vya ujenzi chakavu, kula njama na kuhamisha mabilioni ya fedha kinyume cha masharti ya kifungu cha 156 cha kanuni za Fedha za Umma za mwaka 2001.

Akifafanua mashtaka hayo, katika shtaka la kwanza, Kessy alidai kuwa Machi 5, 2009 washtakiwa wote wakiwa ni wajumbe wa Bodi ya Zabuni ya Suma JKT, kwa makusudi walitumia vibaya madaraka yao kwa kupitisha uamuzi wa kununua magari ya mtumba na vifaa vya ujenzi vilivyotumika.

Alidai kuwa walitenda hayo bila mamlaka ya Bodi ya Wakurugenzi wa Takopa. Takopa ni muungano wa kampuni mbili za ujenzi ya Korea  zilizoingia ubia na  Suma JKT

Jumanne, 25 Septemba 2012

RECHO, DIAMOND NA LINA WATUNDIKA PICHA ZAO BBM.

Recho Atoa Ufafanuzi wa Picha tuliyoweka jana

Jana kupitia mitandao ya jamii, kulikua na mzunguko wa picha hii kila kona ya mitandao hiyo, huku ikiwaacha mashabiki kujiuliza maswali mengi na wengine kudai kuwa inawezekana kuna watu tu wameamua ku edit picha kwa madhumuni ya kuwachafu wasanii hawao ambae ni Lina kushoto, Recho kulia na Diamond.
kupitia simu tumefanikiwa kumpata Recho ambae yupo mkoani Iringa kwa ajili ya show ya leo na haya ndio aliyoyasema.
"hiyo picha ni hali tu ya kawaida, na wala hatukua peke yetu tulikuwa na wasanii wenzetu na presenter wengine tulikuwa tunaogelea,na tulikua tunapiga picha ndio, so ni bahati mbaya tu diamond kutushika sisi vile alikua anajiweka sawa tu sema mpiga picha ndo aliwahi kupiga, bahati mbaya tu ndio mtu akaziweka kwenye bbm ndio ikafika huko.
tulikua sehem to have fan tu, tunaogelea so nikitu ambacho hata mwenyewe sijakipenda kwasababu si tumefanya vile kwa sababu yetu wenyewe ila mwingine anachukua na kuanza kusambaza sio vizuri"
msikilize hapa chini

MAPAMBANO DHIDI YA RUSHWA YAMNASA HAKIMU.

HAKIMU WA ILALA ASOMEWA MASHTAKA YA RUSHWA KISUTU.

Hakimu na Rushwa                                                                    

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 Hakimu Mkazi wa Mahakama ya Wilaya ya Ilala Pamela Kalala (kushoto),akitoka katika mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu jijini Dar es Salaam jana,baada ya kusomewa shitaka la kuomba rushwa ya Shilingi milioni tatu.Picha na Michael Matemanga

Jumapili, 23 Septemba 2012

LIVERPOOL NA MAN U KUKWAANA NDANI YA OLD TRAFFORD.


Liverpool
Liverpool kucheza na Man United ugenini Old Trafford
Meneja wa klabu ya Liverpool, Brendan Rodgers, ana nia ya kuwashirikisha wachezaji wake wote mahiri katika pambano kubwa la Jumapili wakati klabu kitakapocheza katika uwanja wa ugenini wa Manchester United, Old Trafford.
Meneja huyo alifanya mabadiliko 11 siku ya Alhamisi, wakati timu yake ilipocheza dhidi ya klabu ya Young Boys, katika mechi ya ligi ya Europa, na kuiwezesha Liverpool kuondoka na ushindi.
Kati ya wachezaji waliopumzishwa wakati huo kwa misingi ya kucheza Old Trafford ni pamoja na Steven Gerrard, Luis Suarez na Joe Allen.
Man United, licha ya kutocheza vizuri sana msimu huu, walifanikiwa kuishinda Galatasaray ya Uturuki usiku wa Jumatano, na mbali na kushindwa na Everton katika mechi yao ya kufungua msimu, wameshinda mechi nyingine zote, licha ya mchezo wao wa kutovutia sana kufikia sasa.
Man U inatazamiwa pia kufanya mabadiliko kidogo katika kikosi ambacho kiliishinda Wigan, na Robin van Persie na Patrice Evra wanatazamiwa kushirikishwa katika pambano hilo la nyumbani.
Kuna mapambano mengi ya ligi kuu ya Premier ambayo mara kwa mara hutajwa kama ya kukata na shoka, lakini kati ya yote hayo, pambano la Jumapili kwa urahisi linapata sifa hizo.
Baadhi ya mashabiki wa soka nchini Uingereza wanasema uhasama kati ya Liverpool na Manchester United ulianza tangu nyakati za ujenzi wa mfereji uliokuza biashara za usafiri wa meli kutoka Liverpool hadi Manchester, na ukaanza kuzua uhasama kuanzia masuala ya kiuchumi hadi muziki, lakini zaidi kupita yote, ikawa ni uadui katika soka. Kwa hiyo, Liverpool inapocheza na Manchester United, basi hiyo ni mechi ya kusisimua sana nchini Uingereza

Alhamisi, 20 Septemba 2012

IJUE RATIBA YA MECHI LIGI YA MABINGWA ULAYA.(CHAMPIONS LEAGUE 2012-2013)

Champions League   2012 - 2013
All for this: The trophy is paraded around Stamford Bridge
Group Stage
 Teams
  AC Milan
  Ajax
  Arsenal
  BATE Borisov
  Bayern München
  Benfica
  Borussia Dortmund
  Celtic
  CFR Cluj
  Chelsea
  Dinamo Zagreb
  Dynamo Kyiv
  FC Barcelona
  FC Nordsjælland
  FC Porto
  FC Schalke 04
  Galatasaray
  Juventus
  LOSC Lille Métropole
  Málaga CF
  Manchester City
  Manchester United
  Montpellier Hérault SC
  Olympiacos
  Paris Saint-Germain
  Real Madrid CF
  RSC Anderlecht
  SC Braga
  Shakhtar Donetsk
  Spartak Moskva
  Valencia CF
  Zenit Saint Petersburg
 Group A PldWDLFAPts
 Paris Saint-Germain1100413
 FC Porto1100203
 Dinamo Zagreb1001020
 Dynamo Kyiv1001140

18/09/2012 PSG 4 - 1 Dy. Kyiv
18/09/2012 Dinamo Z 0 - 2 Porto
03/10/2012 Porto -  PSG
03/10/2012 Dy. Kyiv -  Dinamo Z
24/10/2012 Dinamo Z -  PSG
24/10/2012 Porto -  Dy. Kyiv
06/11/2012 PSG -  Dinamo Z
06/11/2012 Dy. Kyiv -  Porto
21/11/2012 Dy. Kyiv -  PSG
21/11/2012 Porto -  Dinamo Z
04/12/2012 PSG -  Porto
04/12/2012 Dinamo Z -  Dy. Kyiv

 Group B PldWDLFAPts
 Arsenal1100213
 FC Schalke 041100213
 Montpellier Hérault SC1001120
 Olympiacos1001120

18/09/2012 Olymp. 1 - 2 Schalke 04
18/09/2012 Montp. 1 - 2 Arsenal
03/10/2012 Schalke 04 -  Montp.
03/10/2012 Arsenal -  Olymp.
24/10/2012 Montp. -  Olymp.
24/10/2012 Arsenal -  Schalke 04
06/11/2012 Olymp. -  Montp.
06/11/2012 Schalke 04 -  Arsenal
21/11/2012 Schalke 04 -  Olymp.
21/11/2012 Arsenal -  Montp.
04/12/2012 Montp. -  Schalke 04
04/12/2012 Olymp. -  Arsenal

 Group C PldWDLFAPts
 Málaga CF1100303
 AC Milan1010001
 RSC Anderlecht1010001
 Zenit Saint Petersburg1001030

18/09/2012 Milan 0 - 0 Anderlecht
18/09/2012 Malaga 3 - 0 Zenit
03/10/2012 Zenit -  Milan
03/10/2012 Anderlecht -  Malaga
24/10/2012 Zenit -  Anderlecht
24/10/2012 Malaga -  Milan
06/11/2012 Milan -  Malaga
06/11/2012 Anderlecht -  Zenit
21/11/2012 Zenit -  Malaga
21/11/2012 Anderlecht -  Milan
04/12/2012 Milan -  Zenit
04/12/2012 Malaga -  Anderlecht

 Group D PldWDLFAPts
 Real Madrid CF1100323
 Borussia Dortmund1100103
 Manchester City1001230
 Ajax1001010

18/09/2012 Real 3 - 2 Man City
18/09/2012 Dortmund 1 - 0 Ajax
03/10/2012 Ajax -  Real
03/10/2012 Man City -  Dortmund
24/10/2012 Dortmund -  Real
24/10/2012 Ajax -  Man City
06/11/2012 Real -  Dortmund
06/11/2012 Man City -  Ajax
21/11/2012 Man City -  Real
21/11/2012 Ajax -  Dortmund
04/12/2012 Real -  Ajax
04/12/2012 Dortmund -  Man City

 Group E PldWDLFAPts
 Shakhtar Donetsk1100203
 Juventus1010221
 Chelsea1010221
 FC Nordsjælland 1001020

19/09/2012 Shakhtar 2 - 0 FCN
19/09/2012 Chelsea 2 - 2 Juventus
02/10/2012 Juventus -  Shakhtar
02/10/2012 FCN -  Chelsea
23/10/2012 FCN -  Juventus
23/10/2012 Shakhtar -  Chelsea
07/11/2012 Juventus -  FCN
07/11/2012 Chelsea -  Shakhtar
20/11/2012 FCN -  Shakhtar
20/11/2012 Juventus -  Chelsea
05/12/2012 Shakhtar -  Juventus
05/12/2012 Chelsea -  FCN

 Group F PldWDLFAPts
 BATE Borisov1100313
 Bayern München1100213
 Valencia CF1001120
 LOSC Lille Métropole1001130

19/09/2012 Bayern 2 - 1 Valencia
19/09/2012 Lille 1 - 3 BATE
02/10/2012 BATE -  Bayern
02/10/2012 Valencia -  Lille
23/10/2012 Lille -  Bayern
23/10/2012 BATE -  Valencia
07/11/2012 Bayern -  Lille
07/11/2012 Valencia -  BATE
20/11/2012 Valencia -  Bayern
20/11/2012 BATE -  Lille
05/12/2012 Bayern -  BATE
05/12/2012 Lille -  Valencia

 Group G PldWDLFAPts
 FC Barcelona1100323
 Benfica1010001
 Celtic1010001
 Spartak Moskva1001230

19/09/2012 Celtic 0 - 0 Benfica
19/09/2012 Barca 3 - 2 Spartak
02/10/2012 Spartak -  Celtic
02/10/2012 Benfica -  Barca
23/10/2012 Spartak -  Benfica
23/10/2012 Barca -  Celtic
07/11/2012 Benfica -  Spartak
07/11/2012 Celtic -  Barca
20/11/2012 Spartak -  Barca
20/11/2012 Benfica -  Celtic
05/12/2012 Celtic -  Spartak
05/12/2012 Barca -  Benfica

 Group H PldWDLFAPts
 CFR Cluj1100203
 Manchester United1100103
 Galatasaray1001010
 SC Braga1001020

19/09/2012 Braga 0 - 2 CFR Cluj
19/09/2012 Man Utd 1 - 0 Gala
02/10/2012 Gala -  Braga
02/10/2012 CFR Cluj -  Man Utd
23/10/2012 Gala -  CFR Cluj
23/10/2012 Man Utd -  Braga
07/11/2012 CFR Cluj -  Gala
07/11/2012 Gala -  Man Utd
20/11/2012 CFR Cluj -  Braga
20/11/2012 Braga -  Man Utd
05/12/2012 Braga -  Gala
05/12/2012 Man Utd -  CFR Cluj