Jumamosi, 23 Machi 2013

MKURUGENZI WA ZAMANI WA BODI YA KAHAWA AENDA JELA MIAKA SABA KWA MAKOSA YA RUSHWA.

 Moshi. Mkurugenzi Mkuu wa zamani wa Bodi ya Kahawa Tanzania (TCB), Leslie Omari, amehukumiwa kifungo cha miaka saba jela baada ya kupatikana hatia katika tuhuma zinazoangukia katika makosa ya vitendo vya ufisadi.

Mbali na kifungo hicho, Mahakama pia imemwamuru mshtakiwa kuilipa Benki ya Exim Sh330 milioni, ambazo kampuni yake binafsi ya African Consulting Group (ACGL), ilikopa kwa kutumia dhamana ya jengo la makao makuu ya TCB.

Leslie Omari

Hukumu hiyo iliyokuwa ikivuta hisia za ndugu, jamaa na marafiki wakiwamo watumishi wa TCB, ilitolewa jana na Hakimu Mkazi Mfawidhi wa Mkoa wa Kilimanjaro, Simon Kobelo, huku mkurugenzi huyo akiwa haamini kilichotokea.

Hata hivyo, Hakimu Kobelo alimwachia huru mshtakiwa wa pili katika kesi hiyo, Shaddy Kyambile ambaye wakati makosa hayo yakitendeka mwaka 2003, alikuwa Mkurugenzi wa Fedha wa Bodi ya Kahawa yenye makao yake makuu mjini Moshi.

Hakimu Kobelo alisema anakubaliana na utetezi wa Kyambile kuwa alielekezwa na bosi wake (Omari) kusaini nyaraka za kuidhinisha hati za Jengo la Kahawa, ili zitumike kama dhamana kuikopesha ACGL.

Mkurugenzi huyo mkuu wa zamani, ni miongoni mwa wanahisa wa ACGL, akimiliki asilimia 25 ya hisa.

“Mshtakiwa wa pili alisaini nyaraka kwa maelekezo ya bosi wake (Omari) ambaye alimwambia uamuzi wa kuidhamini ACGL ulishapitishwa na bodi ya wakurugenzi wakati si kweli,”alisema.

Akichambua ushahidi huo, hakimu huyo alisema utetezi wa Kyambile unaungwa mkono na maelezo ya kukiri ambayo Omari aliyaandika akisema yeye ndiye aliyemtaka Kyambile kusaini hati hizo.

Kyambile aliyekuwa akitetewa na wakili mashuhuri wa mjini Moshi, Godwin Sandi kwa sasa ni Mkurugenzi wa Fedha wa Mamlaka ya Uendelezaji Bonde la Ngorongoro (NCAA).

Akichambua ushahidi uliomtia hatiani mkurugenzi huyo, Hakimu Kobelo alisema ushahidi umethibitisha kuwa ni mhusika mkuu wa ACGL na alikuwa miongoni mwa watia saini benki.

Alifafanua kuwa mahakama imemtia hatiani mkurugenzi huyo mkuu kwa makosa mawili moja likiwa ni la matumizi mabaya ya ofisi na lingine la kutumia madaraka yake kujipatia manufaa.

“Japokuwa kwenye utetezi wake (Omari), alikana saini zake na mwandiko wake katika nyaraka mbalimbali, lakini teknolojia ya kisasa, imethibitisha kuwa ni saini yake na mwandiko ni wake,” alisema Hakimu Kobelo alisema katika shtaka la tatu, mshtakiwa atatumikia kifungo cha miaka mitatu na shtaka la nne atatumikia kifungo cha miaka minne. Hata hivyo, Hakimu alisema kwa kuwa vifungo hivyo viwili vitatumikiwa kwa pamoja, basi mshitakiwa atatumikia kifungo cha miaka minne jela na kuilipa Exim Bank Sh330 milioni ambazo ACGL ilizokopa. Kabla ya hukumu hiyo, Mwendesha Mashtaka wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru),Maghela Ndimbo aliiomba Mahakama itoe adhabu kali iwe fundisho kwa watumishi wengine wa umma wanaotumia vibaya madakara yao katika utumishi wa umma. Pia aliiomba Mahakama hiyo imwamuru mshtakiwa kuilipa Benki ya Exim mkopo ambao ACGL ilikopa mwaka 2003 ambao hadi kufikia mwaka 2009 umefikia Sh729.4 milioni pamoja na riba. Kabla ya hukumu hiyo, wakili aliyekuwa akimtetea mkurugenzi huyo, Elikunda Kipoko, aliiomba Mahakama impungizie adhabu mteja wake kutokana na umri, na ni baba anayetegemewa na familia. Baada ya hukumu hiyo, ndugu, jamaa na marafiki wa mshtakiwa aliyeachiwa huru, walijitokeza na kumbkumbatia kwa furaha. Kwa upande wake, Omari hakuaini kilichotokea na hivyo akalazimika kumuuliza wakili wake “Sikuelewa hivi hakimu amesema nini kuhusu mimi.’ Akiwa kizimbani baada ya hakimu tamka kuwa ametiwa hatiani, mkurugenzi huyo wa zamani wa TCB, alishika kichwa kuashiria kutoamini kwake kauli hiyo. Hukumu hiyo imeonyesha kutetemesha watu na hasa ndani ya Bodi ya kahawa Tanzania ambako baadhi ya watu walikuwa wakipiga simu mjini Moshi kutaka kujua kilichokea katika Mahakama ya Hakimu Mkazi.
Chanzo; Gazeti la Mwananchi 

Jumatatu, 18 Machi 2013

ASKARI TRAFIKI WA KIKE AGONGWA NA VX AKIWA ANAONGOZA MSAFARA BARABARANI ENEO LA BAMAGA DAR ES SALAAM . INADHANIWA AMEFARIKI HAPOHAPO.



Baadhi ya wananchi waliofika eneo la tukio.
Hali ilivyokuwa eneo la tukio baada ya ajali hiyo.

Trafiki mmoja ambaye amefahamika kwa jina moja la Elikiza, muda huu amegongwa na gari aina ya VX ambayo haikujulikana namba na inadhaniwa kuwa amekufa papo hapo wakati akiongoza magari eneo la mataa ya Bamaga, Mwenge jijini Dar es Salaam.

Taarifa zilizopatikana eneo la tukio zinadai kuwa Trafiki huyo alikuwa akiongoza msafara na baada ya msafara huo, aliruhusu magari mengine yaendelee na safari ndipo ghafla gari lilipotoka upande wa pili na kumgonga.
(Picha na Shauri Kati / GPL)

Jumapili, 17 Machi 2013

DEREVA WA DALADALA KAPIGWA RISASI AKIWA KWENYE FOLENI SINZA JUZI


Tukio lilitokea Ijumaa usiku kwenye saa tatu kasoro Sinza Kumekucha Dar es salaam karibu na kanisa la KKKT ambapo ilikua ghafla mlio wa risasi ukasikika ikiwa imelengwa kwa dereva wa daladala.

Watu waliokuwepo karibu wamesema dereva wa hii daladala anadaiwa kumkosea na kumkasirisha mtu wa pikipiki alipokua kwenye foleni.

Ghafla mtu huyo wa pikipiki ambae hakufahamika akiwa amebeba abiria inadaiwa alipita kwa mbele akachomoa bastola na kupiga risasi na kuondoka.

Inadaiwa dereva wa daladala aliepigwa risasi kichwani, alifariki muda mfupi baada ya tukio hilo huku watu wakishuhudia abiria mbalimbali wakitokea madirishani na wengine wakitoa vitu vyao kupitia madirishani.
credits;mpekuzi

RIPOTI MAALUMU KUHUSU KUKAMATWA KWA KIJANA ALIYEREKODI VIDEO YA LWAKATARE.

Rwakatare(mwenye kofia)

MTU mmoja aliyetambulika kwa jina la Joseph Ludovick, amekamatwa na Jeshi la Polisi akihusishwa na matukio ya kigaidi ambayo yamelitikisa taifa katika siku za karibuni.

Habari za kuaminika zilizozifikia MTANZANIA Jumapili zimeeleza kuwa, Tume ya watu 12 iliyoundwa na serikali kupitia vyombo vyake vya usalama kuchunguza tukio la kutekwa na kuteswa kinyama kwa Mhariri Mtendaji wa Kampuni ya New Habari (2006) Ltd. Absalom Kibanda, imemkamata Ludovick akiwa mkoani Iringa.

Kwamba, Ludovick amekamatwa na makachero wa polisi baada ya kupatikana kwa taarifa zinazomhusisha kupanga njama za kudhuru watu na pia kuwepo kwa mazingira yenye shaka kuhusu mwenendo wake usiku wa tukio la kutekwa kwa Kibanda.

Hata hivyo, taarifa nyingine zilizopatikana zinadaiwa kuwa kukamatwa kwa Ludovick, ambaye pia anadaiwa kuwa mfanyakazi wa Idara ya Usalama wa Taifa, ni mkakati unaoratibiwa kwa umakini wenye lengo la kupoteza mwelekeo wa uchunguzi wa tukio la kutekwa na kuteswa kinyama Kibanda.

Kibanda alitekwa na kujeruhiwa usiku wa kuakia Machi 6 mwaka huu, nyumbani kwake Mbezi, jijini Dar es Salaam, akiwa ndani ya gari lake akisubiri kufunguliwa geti aingie ndani.

Katika tukio hilo, Kibanda alijeruhiwa kwa kupigwa mapanga kichwani, kung’olewa meno na kucha, kutobolewa jicho na kunyofolewa kidole.

Taarifa zilizopatikana jana kutoka ndani ya Jeshi la Polisi zilieleza kuwa Ludovick, ambaye ni mkazi wa Jijini Dar es Salaam, alikamatwa juzi akiwa mkoani Iringa.

Habari za kukamatwa kwa Ludovick zilianza kuenea tangu juzi usiku katika mitandao mbalimbali ya kijamii, kabla ya jana kuthibitishwa na polisi.

Hata hivyo, Jeshi la Polisi kupitia kwa viongozi wake wakuu, akiwemo, Mkuu wa jeshi hilo, Inspekta Jenerali (IGP), Said Mwema, walikwepa kuzungumzia tukio hilo.

Msemaji wa Jeshi hilo, Advera Senso, alipotafutwa na MTANZANIA Jumapili kupitia simu yake ya kiganjani ili kuthibitisha kukamatwa kwa Ludovick alishindwa kukubali au kukataa.

Senso alilitaka gazeti hili liliache Jeshi la Polisi lifanye uchunguzi wake na kisha kutoa taarifa yake baadaye.

Kuhusishwa kwake na tukio la Kibanda

Habari zilizolifikia gazeti hili zinaeleza kuwa siku na wakati ambao Kibanda alitekwa na kuteswa, Ludovick naye alidai kutekwa na majambazi akiwa eneo la Sinza, jirani na mahali ilipo ofisi ya Kibanda.

Duru za habari zinaeleza kuwa Ludovick alidai kutekwa na watu wasiojulika majira ya saa tano usiku siku ya Jumanne ya Machi 5, mwaka huu, ambapo watekaji wake walimnyang’anya vitu vyake mbalimbali na kumvua nguo zote.

Taarifa hizo zinathibitishwa na mwanablog maarufu, Maggid Mjengwa, ambaye katika andishi lake aliloweka kwenye mitandao ya kijamii jana, anaelezwa kuwa Ludovick, alidai kutekwa na kuvuliwa nguo na kwamba tukio hilo aliripoti katika kituo cha Polisi cha Kigogo.

Kwa mujibu wa maelezo ya Mjengwa kwenye gazeti hili na yale aliyoyaeleza kwenye mtandao wa Jamii Forum, siku ya kutekwa na kuteswa kwa Kibanda alikuwa pamoja na Ludovick kwenye mgahawa wa Rose Garden, ambako walikula chakula jioni kabla ya kuondoka pamoja kwenye gari lake hadi eneo la Sinza Shekilango, alipomuacha akidai kuchukua usafiri wa umma kuelekea nyumbani kwake eneo la Tabata.

Mjengwa anasema baadaye usiku huo, Ludovick alikwenda hadi hoteli aliyofikia eneo la Kariakoo, huku akiwa hana nguo na kumueleza kuwa alitekwa na majambazi muda mfupi baada ya kuachana naye.

Anasema taarifa za kutekwa kwake (Ludovick) aliziripoti katika kituo cha Polisi Kigogo, ingawa kwa mujibu wa maelezo aliyompa Mjengwa ni kwamba alipofika Shekilango, alichukua bajaj ambayo alipanda na watu wengine wawili, yeye akiwa katikati na alipofika katika eneo la Relini Tabata alihisi watu aliokuwa nao ni majambazi.

Hata hivyo, haijajulikana mara moja ni kwa nini akiwa alitekwa eneo la Relini, alikwenda kuripoti tukio hilo katika kituo cha Polisi cha Kigogo.

Pia haijajulikana sababu za kukimbilia hotelini alikofikia Mjengwa badala ya nyumbani kwake, Tabata.

Maswali hayo pia yamempatia kigugumizi Mjengwa, ambaye hata hivyo anakiri kumfahamu Ludovick anaeleza kuwa amekuwa akimsaidia baadhi ya kazi zake za kihabari, lakini anasema hamfahamu sana.

Ludovick ni miongoni mwa watu waliofika katika Hospitali ya Muhimbili asubuhi kumjulia hali Kibanda, na alikaa hadi Kibanda anasafirishwa kwenda nchini Afrika Kusini kwa ajili ya matibabu.

Ahusishwa na video ya Lwakatare

Habari zaidi zilizolifikia MTANZANIA Jumapili, zinadai kuwa Ludovick ndiye mtu aliyerekodi video ambayo Mkurugenzi wa Ulinzi na Usalama wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Wilfred Lwakatare, anaonekana akipanga mipango ya kudhuru watu mbalimbali, wakiwemo waandishi wa habari.

Wapasha habari wetu wanaeleza kuwa Ludovick ndiye mtu ambaye sauti yake inasikika katika video hiyo, hata hivyo habari hizo hazijathibitishwa na Jeshi la Polisi.

Katika video hiyo iliyosababisha Lwakatare atiwe nguvuni na Polisi hadi sasa, Ludovick anadaiwa kuwa ndiye mtu ambaye alikuwa akimuuliza maswali Lwakatare, wakati wakiandaa mipango hiyo.

Watu wa karibu na Ludovick waliliambia gazeti hili kuwa, Lwakatare na Ludovick wana uhusiano wa karibu na kwamba wote ni wenyeji wa Mkoa wa Kagera.

Kwa mujibu wa watu hao, ukaribu kati ya Ludovick na Lwakatare ni wa muda mrefu na amepata kumsaidia kufanya kampeni za kuwania ubunge wa Jimbo la Bukoba Mjini mwaka 2000.

Wakati huo huo, inadaiwa kuwa Lwakatare mwenyewe amekiri kuwa mtu anayeonekana akizungumza katika mkanda wa video maneno ya kupanga matukio ya utekaji ni yeye na pale anapoonekana akizungumza ni nyumbani kwake, lakini amekataa kwamba maneno anayozungumza si yeye.

Ludovick ni nani?

Ludovick, mbali na kuwa na ukaribu na Lwakatare, pia ni mtu wa karibu na Mjengwa, akimsaidia katika shughuli mbalimbali hususani katika blog yake.

Kuna taarifa ambazo hazijathibitishwa kwamba Ludovick ni mtu wa idara ya usalama wa taifa na watu ambao wako naye karibu wanasema hawajui anafanya kazi gani zaidi.

Alipoulizwa ni kazi gani ambayo Ludovick anafanya, Mjengwa alisema hajui.

Ila katika maelezo yake aliyoandika kupitia kwenye mtandao wa Jamii Forum, Mjengwa anasema anamfahamu Ludovick tangu akiwa Chuo Kikuu (DUCE) na kwamba ni mmoja wa Watanzania wengi waliomfahamu kupitia kazi zake magazetini.

Haijaeleweka mara moja uhusiano wake na Lwakatare ni wa aina gani na katika kazi gani.
Credits;freebongo

Alhamisi, 14 Machi 2013

WAISLAMU WAONYA KAULI ZA UCHOCHEZI ZINAZOTOLEWA NA VIONGOZI DHIDI YAO.

 

Mchungaji Christopher Mtikila. 

Na Florence Majani na Mussa Mwangoka 
Dar es Salaam.  Wakati Kiongozi wa Chama cha Democratic (DP), Mchungaji Christopher Mtikila akitiwa mbaroni kwa tuhuma za uchochezi wa kidini, viongozi wa Jumuiya  ya Kiislamu Tanzania wametoa tamko na kusema kuwa baadhi ya kauli za viongozi wa Serikali na viongozi wa dini zina mwelekeo wa kukuza mfarakano wa kidini kuliko kuleta maelewano.
Wiki iliyopita Mchungaji Mtikila alikamatwa mkoani Rukwa akituhumiwa kuwahamasisha Wakristo wawavamie Waislamu.
Kamanda wa Polisi mkoani Rukwa, Jacob Mwaruanda alisema Mchungaji Mtikila alichochea uhasama kwa kuwaeleza viongozi wa Kikristo kuwa, wamekuwa wakionewa na Waislamu kutokana na matukio yanayoendelea kutokea hapa nchi.
Katika tamko lao, viongozi wa  Kiislamu walisema kuwa mara nyingi kauli  za viongozi wa dini na Serikali hazina nia njema bali zimekuwa za kibaguzi au za kiupendeleo.
“ Imekuwa ni kawaida kila anaposhambuliwa au kuuawa Padri baadhi ya viongozi wa Serikali, na wale wa Kikristo, vyombo vya habari, baadhi ya asasi na taasisi za kiraia wamekuwa wakiwanyooshea vidole na kuelekeza lawama zao kwa jamii ya Waislamu,” lilisema tamko hilo.
Katika tamko hilo Jumuiya ya Waislamu ilieleza kuwa Waislamu wamekuwa wakinyooshewa vidole kutokana na matukio hayo pasipo kuwa na ushahidi.
Iliongeza kuwa wamekuwa wakishutumiwa kuhusika katika matukio kabla hata ya  uchunguzi wa vyombo vya usalama na polisi kufanyika.
Tamko hilo lilisema kuwa serikali kupitia waziri wa mambo ya ndani ilitoa kauli kuwa mauaji ya padri huyo ni matokeo ya kazi za ugaidi.
Tamko hilo lilisisitiza kuwa linaungana na wapenda amani wote kulaani mauaji, manyanyaso  na udhalilishaji wa aina yoyote unaowalenga viongozi wa dini.
Jumuiya hiyo imewataka viongozi wa dini na Serikali kuhakikisha wanahimiza  amani na mshikamano badala ya kuwa vyanzo vya kuchochea vurugu.
Wamesema hawatafumbia macho tabia ya kuendelea kunyoshewa vidole Waislamu kila linapotokea tukio la uvunjifu wa amani nchini na wamewataka Watazania wote kwa umoja wao kusimamia ushirikiano na kuiimba amani ili kulinusuru taifa na aina yoyote ya vurugu.
Chanzo; Gazeti la Mwananchi

JORGE BERGOGLIO TOKA ARGENTINA ACHAGULIWA KUWA KIONGOZI WA KANISA KATOLIKI DUNIANI.ACHAGUA JINA LA PAPA FRANCIS.



Jesuit Cardinal Jorge Bergoglio wa Buenos Aires amechaguliwa kuongoza Wakatoliki billioni moja kama Papa Francis I.

Ni Baba Mtakatifu wa kwanza kutoka Amerika ya Kusini. Kwenye hotuba yake ya kwanza amwombea Benedict, aomba Kanisa "litembee pamoja katika imani".

Ametoa baraka yake ya kwanza ya umma saa nne unusu kwa saa za Afrika Mashariki. Awaomba waumini wamwombee.Wachambuzi wasema Francis ni Papa "mnyenyekevu."

Jumamosi, 9 Machi 2013

UHURU KENYATTA ATANGAZWA KUWA MSHINDI WA URAIS WA KENYA KWA ASILIMIA 50.07

MWENYEKITI WA TUME YA UCHAGUZI NA MIPAKA YA KENYA I.E.B.C BW. HASSAN ISACK AMEMTANGAZA  BW. UHURU KENYATTA KUWA NDIYE MSHINDI WA URAIS KATIKA UCHAGUZI WA MWAKA HUU 2013 BAADA  YA KUPATA USHINDI WA  ASILIMIA 50.07 HIVYO KUFANYA UCHAGUZI WA AWAMU YA PILI USIWEPO. JAMES KIAPI, MARTHA KALUA, MOHAMED DIDA , MUSARIA, KUVUITO, PETER KENETH, RAILA ODINGA AND UHURU KENYATTA THE WINNER.

MCHAKATO WA KUMPATA PAPA MPYA WAENDELE HUKO VATCAN CITY.

Maandalizi ya kumteua Papa mpya yanaendelea.

Mkutano rasmi wa makadinali mjini Vatican kumchagua Baba Mtakatifu mpya unatarajiwa baadae mwezi huu.
Mkutano rasmi wa makadinali mjini Vatican kumchagua Baba Mtakatifu mpya unatarajiwa baadae mwezi huu.
Yeyote atakayechaguliwa kuwa kiongozi wa kanisa Katoliki duniani atakabiliana na changamoto nyingi.
Baadhi ya nchi za Ulaya zilizokuwa vinara kueneza injili katika nchi zinazoendelea, kwa sasa zina upungufu wa makasisi katika makanisa yao.
Nchini Ufaransa na Ireland, sasa wameligeukia bara la Africa - ambapo ukatoliki unakuwa, kuchukua mapadre. Huyu ni mmoja wa mapadre hao

Jumapili, 3 Machi 2013

REAL MADRID YAONESHA UBABE TENA KWA BARCELONA, YASHINDA 2-1

 Ian Ladyman In Madrid
With the return leg of their Champions League tie with Manchester United on the horizon, momentum is beginning to gather within the ranks of Real Madrid.
Minutes before the referee called time on a second Real victory over Barcelona in five days here this afternoon, a cry of 'Jose Mourinho, Jose Mourinho' began to drift round the Bernabeu.
As the observer sitting to my right in the press box murmured: 'We haven’t heard that for a while.'
This is what it’s like for a coach in Spain and especially here in Madrid.
Winning moment: Real Madrid captain Sergio Ramos headed the winner with nine minutes remaining
Winning moment: Real Madrid captain Sergio Ramos headed the winner with nine minutes remaining
Joy unconfined: Ramos celebrates with Luka Modric, who swung in the corner for the winning goal
Joy unconfined: Ramos celebrates with Luka Modric, who swung in the corner for the winning goal
Delight: The Real Madrid fans celebrate a second win over Barcelona in five days
Delight: The Real Madrid fans celebrate a second win over Barcelona in five days

Match Facts


Real Madrid: Lopez; Ramos, Varane, Pepe, Coentrao (Arbeloa 70); Essien, Modric; Callejon, Kaka (Ronaldo 59), Morata; Benzema (Khedira 57)
Substitutes: Adan, Ozil, Carvalho, Higuain, Arbeloa
Scorer: Benzema 5, Ramos 81
Booked: Ramos, Coentrao, Morata
Barcelona: Valdes; Alba, Piqué, Mascherano, Alves; Busquets, Thiago (Tello 87), Iniesta; Villa (Alexis 67), Messi,  Pedro (Adriano 76)
Substitutes: Pinto, Puyol, Song, Fabregas
Scorer: Messi 17
Booked: Alba, Pique, Thiago, Messi, Alves
Sent off: Valdes
Mourinho has spent much of this season trying to ignore the dissenting voices in the Madrid media and among the Madridistas as memories of last season’s La Liga title have disappeared in the face of such a limp attempt to win it again.
Nevertheless, Madrid can now smell possibility in the Champions League, the competition they want to win more than any other after more than a decade without success.
Certainly, they are improving. This was an odd game at times as a Real team deprived of seven of its regular starters – including Cristiano Ronaldo – faced their great rivals from Barcelona in the glare of a surprisingly powerful March sun.
At half-time, it looked as though it may drift in to stalemate. Karim Benzema scored in the sixth minute from an Alvaro Morata cross and then Lionel Messi equalised with his 50th goal of the Spanish season, scoring with his left foot after Dani Alves played him through.
That apart there had been little to get excited about but, as is often the way between these two teams, things began to get a little tense and fractious in the second half and as the competitiveness of the game increased it was Real who seemed ready for a real contest.
Certainly it helped when Ronaldo came on with half an hour left. Within 15 minutes of his arrival, he had hit the side netting and brought a save from Victor Valdes with a free-kick. Before the game was over he was to hit the bar from 25 yards too.
Equaliser: Lionel Messi levelled the scores for Barcelona on 17 minutes with his 50th goal of the season
Equaliser: Lionel Messi levelled the scores for Barcelona on 17 minutes with his 50th goal of the season

Lionel Messi scores for Barcelona
Ronaldo’s very presence in Mourinho’s team serves to lift them. It is quite remarkable to watch. And even though he was not involved in the winning goal that arrived with six minutes left it came after a passage of play that he had been at the very heart of.
Sergio Ramos it was who headed in the goal from a Luka Modric corner to spark some quite enthusiastic celebrations on the field and off it. There was still time for the referee to wave away what seemed to be decent penalty appeals for a Ramos foul on Adriano and Barcelona goalkeeper Valdes was sent off after the final whistle for the vociferous manner of his protests.
No doubt that ‘injustice’ will dominate the headlines in the Barcelona sports papers tomorrow morning. Here in Madrid, though, it will all be about Tuesday night’s visit to Old Trafford. They may trail Barcelona by 13 points in the league but in Europe it must be said that they look ready.
Assistant coach Aitor Karanka was delighted with the performances of Real Madrid's fringe players after first-team coach Jose Mourinho made seven changes from the side that beat the Catalans 3-1 on Tuesday at the Camp Nou in the Copa del Rey.
Karanka said: 'You need all your players to deliver in a big game like this, including the ones who play less often.
'Of all the performances of the team, I was particularly impressed with those players. The team have shown that, whoever is playing, they deserve to be trusted.'
Opener: Karim Benzema scored after five minutes to give Real the lead, to the delight of the packed Bernabeu crowd
Opener: Karim Benzema scored after five minutes to give Real the lead, to the delight of the packed Bernabeu crowd

Karim Benzema celebrates scoring the opening goal
Karim Benzema celebrates scoring the opening goal
However, Karanka warned his players against being complacent after the consecutive victories over their biggest rivals, ahead of Tuesday's Champions League last-16 second leg encounter at Manchester United.
'We have to be happy with the result but if we think we have done something extraordinary we could end up regretting it on Tuesday,' he said.
'There's no champagne here to celebrate anything, all we'll be doing is working hard while remaining excited about the rest of the season We have to keep going in the same direction.'
Karanka explained that Madrid dealt with the pressure of having the three decisive games - the two with Barcelona and one at Manchester United - in such a short space of time by just focusing on their day-to-day work.
'We work hard every day and these games make us work even harder,' he added. 'Everyone was saying that the season could be over this week but we haven't let us affect us.
'We just work to make sure the team is as good as possible.'
Barcelona assistant coach Jordi Roura was happy with his team's performance, despite the defeat.
He said: 'We came here to try and increase our advantage (over Madrid in the Primera Division table) and we have to be happy with the team's attitude, we stood up and were counted and had chances to win at a very difficult stadium.
'We could have got something from the game, but we are still alive and well.'
Roura did not comment on goalkeeper Victor Valdes being sent off at the final whistle for arguing with the referee, simply saying: 'I went straight to the dressing room after the game and I didn't see anything.'
Roura did not complain outright about the penalty which Adriano was denied in the final minutes of the game after a challenge by Sergio Ramos, but implied he was not happy with the decision.
He said: 'I don't have anything more to say about the refereeing. I spoke during the week and to me it is perfectly clear if you look at the replays.'
Barcelona are now 13 points clear of Madrid in the Primera Division table and 12 clear of Atletico Madrid, who play Malaga tomorrow.
Roura stressed the need for his team to return to winning ways and hold onto, or increase, their lead at the top from now until the end of the season.
'The important thing is now to keep trying to pick up points, we still have a significant advantage and we will try to extend it even further,' he added.
Benched! Ronaldo started the match among the substitutes, but came on with half an hour to play to great effect
Benched! Ronaldo started the match among the substitutes, but came on with half an hour to play to great effect

FATOU BENSOUDA ATEMBELEA TANZANIA, NI MWENDESHA MSHTAKA MKUU WA ICC



Rais Jakaya Kikwete akiwa katika picha ya pamoja na Mwendesha Mashtaka Mkuu wa Mahakama ya Uhalifu wa Kimataifa (ICC), Fatou Bensouda alipofika Ikulu jijini Dar es Salaam 
Na Fidelis Butahe
Mwendesha Mashtaka Mkuu wa Mahakama ya Uhalifu wa Kimataifa (ICC), Fatou Bensouda, ametua nchini jana na kufanya mazungumzo na Rais Jakaya Kikwete, Ikulu Dar es Salaam.

Hatua hiyo ya ICC imekuja ikiwa ni miezi sita tangu Serikali ya Tanzania ilipopelekwa katika mahakama hiyo, iliyoko The Hague,  Uholanzi kwa madai ya kukiuka haki za binadamu.

Malalamiko hayo maalumu yalipelekwa ICC na Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu (LHRC), Septemba 28 mwaka jana, baada ya kutokea kwa mauaji ya aliyekuwa mwandishi wa habari wa Kituo cha Televisheni cha Channel Ten, Daudi Mwangosi na watu wengine 23.

Taarifa ya LHRC ilieleza kuwa pamoja na watu hao kuuawa, Serikali ilishindwa kuwachukulia hatua wahusika.

Mbali na kuishtaki Serikali ICC, kituo hicho cha Sheria na Haki za Binadamu pia kilipeleka mashtaka kwenye Tume ya Afrika ya Haki za Binadamu.



Mkurugenzi Mtendaji wa kituo hicho, Dk Hellen Kijo-Bisimba, alisema kuwa walifungua mashtaka hayo ili kuzitaka mamlaka hizo za kimataifa kufanya uchunguzi na kuichukulia hatua stahiki za kisheria dhidi ya Serikali ya Tanzania.

Jana Rais Jakaya Kikwete alikutana na Bensouda na kufanya mazungumzo na baadaye walipiga picha za pamoja nje ya Viwanja vya Ikulu,  akiwa pamoja na Mwanasheria Mkuu wa Serikali (AG), Jaji Frederick Werema, Naibu Waziri wa Katiba na Sheria, Angellah Kairuki na Mkurugenzi wa Mashtaka (DPP), Eliezer Feleshi.

Katika maelezo yake Bisimba alisema: “Tumepeleka mashtaka 24 ICC tangu Septemba 28 mwaka huu, ambayo yanahitajika kufanyiwa uchunguzi na kuchukua hatua kali dhidi ya Serikali ya Tanzania ambayo imekuwa ikiwalinda viongozi wake wanaokiuka haki za binadamu.”

“Tunatarajia kuona uwajibikaji wa viongozi wote wa Serikali na vyombo vya dola waliohusika kwa njia yoyote ile. Hatua hizo au uwajibikaji huo ni pamoja na kujiuzulu, kuachishwa kazi na kufikishwa Mahakamani,” aliongeza Dk Bisimba.

Gazeti hili lilipomtafuta Jaji Werema kuzungumzia ujio wa Bensouda alisema kuwa Mwendesha Mashtaka huyo alikuwa mgeni wa Rais Kikwete, hivyo hawezi kueleza kilichozungumzwa.

“Alikuwa mgeni wa Rais, lakini kubwa nililolisikia ni kwamba alikuja kusalimia kwa sababu tangu alipoteuliwa hakuwahi kuja Tanzania,” alisema Werema.

Kama ilivyokuwa kwa Werema, naye Feleshi  alikwepa kuzungumzia ujio huo wa Mwendesha Mashtaka Mkuu wa ICC, huku akisema jambo hilo linaweza kutolewa ufafanuzi na Ikulu.
Kwa Hisani ya Gazeti la Mwananchi.

WADAU WA BLOGU YA MAMBOBADO TUNAWAOMBA RADHI KWA KUTOPOST VITU TULIVYOZOEA KAMA KAWAIDA, HII NI KUTOKANA NA TATIZO LA MITANDAO YETU YA SIMU KUKOSA NGUVU KATIKA HUDUMA YA INTERNET PIA UMEME USIO NA UHAKIKA UNAOTOLEWA NA TANESCO HUKU MAENEO YA NACHINGWEA LINDI, MAMBO YAKITULIA TUTAPATA VITU KAMA KAWA, TCHAO!!!

HALI NI MBAYA JAMANI, HEBU TUTAFAKARI NA PICHA HII TOKA INDIA WAKATI TUNASUBIRI MAMBO YETU YAKAE SAWA, SIKU NJEMA WADAU.