Jumamosi, 16 Novemba 2013

MAREHEMU DK. SENGONDO MVUNGI AMEAGWA LEO VIWANJA VYA KARIMJEE, ANATARAJIWA KUZIKWA KESHO HUKO CHANJALE KISANGARA JUU WILAYANI MWANGA.

 Makamu wa Rais Dkt Gahlib Bilali, Waziri Mkuu Mizengo Pinda, Rais Mstaafu Benjamin Mkapa, Waziri Mkuu Mstaafu na Mwenyekiti wa Tume ya Kurekebisha Katiba Jaji Joseph Warioba, Naibu Waziri wa Sheria na Katiba Mhe Angela Kairuki na Mwenyekiti wa NCCR-Mageuzi Mhe James Mbatia wakiwa katika shughuli za kuaga mwili wa marehemu, Dkt.Sengondo Mvungi,kwenye Viwanja vya Karimjee jijini Dar es Salaam,leo. 
Mapadre wakiendesha misa wakati wa shughuli hiyo leo.
 
 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungani wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akitoa heshima za mwisho mbele ya jeneza lenye mwili wa marehemu, Dkt.Sengondo Mvungi, wakati wa shughuli ya kuagwa mwili huo iliyofanyika kwenye Viwanja vya Karimjee jijini Dar es Salaam,leo.
Waziri Mkuu Mhe Mizengo Pinda  akitoa heshima za mwisho mbele ya jeneza lenye mwili wa marehemu, Dkt.Sengondo Mvungi, wakati wa shughuli ya kuagwa mwili huo iliyofanyika kwenye Viwanja vya Karimjee jijini Dar es Salaam,leo. Picha na OMR

Jumatatu, 11 Novemba 2013

UFILIPINO YAKUMBWA NA KIMBUNGA KIKUBWA SANA KIITWACHO HAIYAN, WAKAZI WAKUMBWA NA HOFU WAKIDHANIA NI TSUNAMI, WAKAZI ZAIDI YA ELFU KUMI WAHOFIWA KUFARIKI.

Picking up the pieces: Some residents try to go about their daily business despite the large-scale destruction
Picking up the pieces: Some residents try to go about their daily business despite the large-scale destruction

Victim
 
 resident recover a body of a victim

Tragedy: Bodies of residents can be seen in the streets of Tacloban, while one local is forced to transport a body in a wheelbarrow




Collapsed: A resident walks past her destroyed home - flattened by piles of wood and branches from nearby trees - in Tacloban city
Collapsed: A resident walks past her destroyed home - flattened by piles of wood and branches from nearby trees - in Tacloban city
 
International Development Secretary Justine Greening has also pledged £6million worth of emergency aid.
She said: 'My thoughts are with the people of the Philippines, in particular those who have lost loved ones. UK support is now under way.
'Many thousands of people in remote, hard-to-reach communities have lost their homes and everything they own. They are living in the open and completely exposed to the elements.
'The absolute priority must be to reach them with shelter and protection as soon as possible.
'UK support will provide urgently needed access to clean water, shelter, household items and blankets,
'We are also sending additional humanitarian experts from the UK to work with the DfID team and international agencies, including ensuring partners are prioritising the protection of vulnerable girls and women.'

Workers: Local Red Cross staff place sand bags on the roof of a house in Danang, Vietnam
Workers: Local Red Cross staff place sand bags on the roof of a house in Danang, Vietnam



Debris: Helicopters hover over the damaged area of Tacloban city, which was battered with strong winds yesterday
Debris: Helicopters hover over the damaged area of Tacloban city, which was battered with strong winds yesterday

Victim: A resident walks past dead bodies that lie on the street in Tacloban city, Leyte province
Victim: A resident walks past dead bodies that lie on the street in Tacloban city, Leyte province
Vice mayor Jim Pe of Coron town on Busuanga, the last island battered by the typhoon, said most of the houses and buildings there had been destroyed or damaged.
Five people drowned in the storm surge and three others are missing. He said: 'It was like a 747 flying just above my roof.' adding that his family and some of his neighbours whose houses were destroyed took shelter in his basement.
In the aftermath, people were seen weeping while retrieving bodies of loved ones inside buildings and on a street that was littered with fallen trees, roofing material and other building parts torn off in the typhoon's fury.
All that was left of one large building whose walls were smashed in were the skeletal remains of its rafters.

Under water: Residents wade through a flooded street in Mindoro, Philippines this morning following the typoon
Under water: Residents wade through a flooded street in Mindoro, Philippines this morning following the typoon

Pile up: Vehicles and rubbish are pictured strewn across a flooded street in Tacloban, Leyte
Pile up: Vehicles and rubbish are pictured strewn across a flooded street in Tacloban, Leyte

Upside down: A devastated airport in Tacloban city, Leyte province - where roofs were ripped on hundreds of houses
Upside down: A devastated airport in Tacloban city, Leyte province - where roofs were ripped on hundreds of houses


 Coron, Palawan
 
 Coron, Palawan

Shock: These two pictures show the devastation in Coron, Palawan where buildings have been flattened, left and right, leaving residents helplessly walking the streets.
 
 

Jumapili, 10 Novemba 2013

PICHA ZA LEO; TUCHEKE KIDOGO NA NDUGU ZETU TOKA INDIA WANAVYOSEMEKANA KUPENDA SANA PIKIPIKI KWA SHUGHULI MBALIMBALI.

Huyu tena akionesha umwamba na uwezo wake wa kuibeba pikipiki kichwani yenye uzito wa zaidi ya kilogramu 120.
Jamaa akirahisisha uchukuzi wa mabomba kwa usafiri wake wa tuktuk. Jumapili njema basi.

Jumamosi, 9 Novemba 2013

JAMANI TUNAKWISHA, AJALI ZA PIKIPIKI ZIMERIPOTIWA SANA JUMA HILI, TUELIMISHANE NA KUKUMBUSHANA KUCHUKUA TAHADHARI.

 
Toyota Land Cruiser linalodaiwa kumgonga muendesha pikipiki aliyetambulika kwa jina moja la Huweso.
 

...Askari wa usalama wa barabarani akichukua maelezo katika eneo la tukio, alielala chini ni Huweso baada ya kupata ajali.

Picha mbili za juu zinaonesha ajali iliyotokea juzi Ihumwa Dodoma ikisababisha vifo vya vijana wawili Ramadhan Lesso na George Lwandala ambao walikuwa wanafunzi wa CBE Dodoma, chanzo cha ajali ni mwendokasi na lori kupaki bila alama zozote kando ya barabara kuu ya Morogoro-Dodoma. Wanafunzi hao waliligonga lori kwa nyuma na kufariki papo hapo.


Ajali nyingine ya pikipiki imetokea juzi huko Geita ikihusisha mwendesha bodaboda na abiria wake wa kike ambao hawakufahamika majina yao kuanguka katikati ya barabara na baadae kukanyagwa na gari aina ya Noah waliyokuwa wanapishana nayo.
RAI
Kila mtu kwa nafasi yake ajaribu kufanya wajibu wake ikiwa ni kuelimisha waendesha bodaboda kwenda kwa mwendo wa tahadhari na wastani ili ikitokea tatizo la ghafla waweze kudhibiti, wenye magari waheshimu wenye vyombo vidogo barabarani kama bajaj na pikipiki pia abiria wajaribu kuwadhibiti madreva wao wanapoona wanaenda kwa kasi sana.

Jumapili, 3 Novemba 2013

MENO YA TEMBO 200(VIPANDE 706) YAKAMATWA JIJINI DAR ES SALAAM KWA WACHINA HUKU WABUNGE WAKICHACHAMAA OPERESHENI MAJANGIRI ISITISHWE.


Meno ya Tembo

Raia watatu wa China wamekamatwa nchini Tanzania kwa kukutwa na meno 706 ya tembo, sawa na tembo 353 waliouawa katika hifadhi mbalimbali nchini humo.
Pia watuhumiwa hao wa Kichina wamekutwa na fedha taslim shilingi milioni 30.2 za Kitanzania, sawa na zaidi ya dola elfu 18 za Kimarekani.
Waliokamatwa na meno hayo ya tembo wametajwa kuwa ni Chen Jinzha, Huang Qin na Xu Fujie wote kutoka mji wa Guangdung nchini China.Waziri wa Maliasili na Utalii, Balozi Khamis Kagasheki akifuatana na kikosi maalum cha polisi, waliwanasa Wachina hao katika makaazi yao jijini Dar es Salaam.
Raia hao wa China wamekuwa wakiishi katika nyumba walimokamata meno ya tembo kwa miaka mingi wakifanya biashara ya kuingiza vitunguu swaumu nchini Tanzania kutoka China huku wakisafirisha nje makombe ya konokono wa baharini.
Akizungumza na waziri Kagasheki, mtuhumiwa Huang Qin amesema shehena yote iliyokamatwa ndani mwake ilikuwa ikiletwa kidogo kidogo na rafiki yake ambaye hakumtaja jina.
Kukamatwa kwa meno haya ya tembo Jumamosi, kumekuja wakati tayari serikali imetangaza kusitisha "Operesheni Tokomeza Ujangili", ambayo ililenga kunusuru wanyama walio hatarini kutoweka kutokana na kuuawa katika hifadhi za taifa nchini Tanzania. Wanyama wanaolengwa zaidi na majangili kutokana na meno yao na pembe ni tembo na faru.
Matukio ya kukamatwa kwa meno ya tembo kutoka Afrika Mashariki yamekuwa yakiripotiwa kila mara. Oktoba, 20, 2012, tani nne za meno ya tembo yenye thamani ya dola milioni 3.4 za Kimarekani yalikamatwa Hong Kong, yakidaiwa kusafirishwa kutoka Kenya na Tanzania.
Pia Agosti 16 mwaka huu polisi wa Uwanja wa Ndege wa Mwalimu Julius Nyerere jijini Dar es Salaam, walimkamata raia mmoja wa Vietnam akiwa na meno ya tembo yenye thamani ya zaidi ya shilingi milioni 18 sawa na dola za Kimarekani zaidi ya elfu 11, yakisafirishwa kwenda nje.

PICHA YA LEO; PUNDA AFE MZIGO UFIKE, UNAONA BAISKELI INAVYOPAKIA INGAWA HAINA BODI!?

Picha ikionesha jinsi baiskeli inavyoweza kubeba mzigo mzito na mwingi mara moja, picha hii imechukuliwa huko India miaka michache iliyopita.

KESI YA BABU SEYA NA PAPII KOCHA YAFANYIWA MAREJEO MAHAKAMA YA RUFAA TANZANIA, VICHEKO AU VILIO TENA VINAKARIBIA. TUWAOMBEE MAMBO YAWE MAZURI.

Stori: Richard Bukos na Denis Mtima MWANAMUZIKI mkongwe wa muziki wa dansi, Nguza Viking maarufu kama Babu Seya na mwanaye Johnson Nguza ‘Papii Kocha’ pamoja na ndugu zao, Jumatano iliyopita walitoka kwa vicheko katika Mahakama ya Rufaa Tanzania baada ya kuridhishwa na utetezi uliotolewa na wakili wao, Mabere Marando, anayepinga hukumu ya kifungo cha maisha jela, waliyopewa wanamuziki hao.


Babu Seya na Papii Kocha wakiwa na furaha wakati wakitoka katika Mahakama ya Rufaa Tanzania.
Mbele ya majaji watatu wa Mahakama hiyo, Marando alikabiliana na timu ya mawakili watano waandamizi wa serikali ambao ni Jackson Brashi, Angaza Mwaipopo, Imaculate Banzi, Joseph Pande na Apimark Mabruk.


Babu Seya (wa pili kulia) na Papii Kocha (wa pili kushoto) wakiwa mahakamani kusikiliza rufaa yao.
Miongoni mwa hoja ambazo Marando alionekana kuwabana mawakili wa serikali ni jinsi Jamhuri ilivyowatia hatiani wateja wake kwa kutumia ushahidi uliotolewa na watoto katika Mahakama ya Hakimu Mkazi ya Kisutu jijini Dar, akisema zipo taratibu za kuchukua katika ushahidi kwa mtoto ikiwemo kurekodiwa, jambo ambalo halikufanyika.


...Wakiwa na furaha wakati wakitoka katika mahakama baada ya kuridhishwa na utetezi uliotolewa na wakili wao, Mabere Marando.
Marando alizidi kuweka wazi kuwa katika ushahidi uliotolewa mahakamani hapo, ulionesha nyumba iliyodaiwa kufanyiwa uhalifu huo ilikuwa na mlango wa siri uliotumiwa na watoto hao kupenya hadi ndani pasipo kuonekana jambo ambalo baadaye lilidhihirika si kweli kwani nyumba hiyo haikuwa na mlango mwingine zaidi ya wa uani na barazani.


Wanahabari wakijaribu kupata matukio katika tukio hilo.
Hata hivyo, jopo la mawakili wa Jamhuri licha ya kukumbana na wakati mgumu kutoka kwa wakili Marando, liliendelea kusisitiza kuwa hukumu iliyotolewa dhidi ya washitakiwa hao ilikuwa sahihi.
Baada ya mawakili hao kusisitiza hivyo Marando alipewa nafasi nyingine ya kutoa utetezi wake, ambapo aliendelea kufafanua makosa mbalimbali yaliyofanyika kuwahukumu wateja wake kwa kutaja vifungu vya sheria ambavyo vilionekana kama kuwasafishia njia wateja wake hao hali iliyozua tabasamu na vicheko mahakamani hapo.


Watoto wawili wa Babu Seya, Nguza Mbangu (kulia) na Francis Nguza (kushoto) wakiwa na nyuso za furaha baada ya kuona kesi ya baba yao na ndugu yao inaelekea pazuri.
Baada ya kupitia marejeo ya kesi hiyo kwa pande hizo mbili, jopo la majaji akiwemo, Salum Masatti liliahirisha kesi hiyo na kusema litapanga siku ya hukumu huku wafungwa hao wakirejeshwa gerezani wakiwa na vicheko vya furaha huku ndugu na jamaa nao wakikumbatiana kwa shangwe.
Credits;globalpublishers.info